• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DC Misungwi atoa siku 20 kwa Halmashauri kuanza kukusanya ushuru wa Masoko yote Misungwi

Imewekwa : January 11th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe, Veronika Kessy aagiza  Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi  kuanza kukusanya Ushuru wa mapato yatokanayo na Masoko   yote kuanzia Februari mosi mwaka huu ili kuongeza mapato ya ndani.

Akizungumza juzi katika kikao cha  tathmini na kupokea taarifa ya uchambuzi wa mfumo wa usimamizi na uendeshaji wa  masoko Wilayani Misungwi iliyotolewa na Ofisi ya Kuzuia na Kupambana na rushwa (TAKUKURU) Wilaya ya Misungwi tarehe 09/01/2023 kwa lengo la kuboresha na kuongeza mapato ya Halmashauri ameeleza kwamba ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halamshauri kupitia Kitengo cha fedha na mapato wanatakiwa kuhakikisha wanasimamia ukusanyaji wa ushuru katika masoko yote ikiwemo  soko la Misungwi. Usagara, Nyashishi, na Bujigwa.

Taarifa ya uchambuzi ya masoko ilibainisha kwamba Menejimenti ya Halmashauri ya Misungwi  kwa muda mrefu sasa  imeshindwa kukusanya kikamilifu ushuru katika masoko hayo  na badala yake Viongozi wa  Serikali za vijiji pamoja na Wananchi wasiokuwa waadilifu wamekuwa wakitoza ushuru huo na mapato husika yamekuwa yakitumika kinyume na taratibu ambapo Halmashauri ndio yenye mamlaka na jukumu katika usimamizi na ukusanyaji ushuru kwenye masoko kwa mujibu wa sheria za fedha.

Mhe Veronika Kessy amekerwa na vitendo vya baadhi ya Viongozi, Wananchi  na Watendaji wasiokuwa waadilifu waaminifu ambao wamekuwa wakikaidi katika kutekeleza shughuli za maendeleo ya Wananchi ambao wengine wamekuwa wakijihusisha na shughuli za Ukusanyaji wa ushuru wa usafi  katika masoko kinyume na sheria na taratibu na kutowasilisha mapato hayo katika mfuko wa Halamsahuri.

Ameelekeza  Jeshi la Polisi Wilaya  ya Misungwi kuwahoji Mwenyekiti na Mtendaji wa Kijiji cha Misungwi na kutoa maelezo ya kina kuhusu ukaidi unaofanywa na Mwenyekiti huyo wa kijiji kwa kutotekeleza maagizo na maelekezo ya mara kwa mara kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri kuhusu kuhusika kwake  kuweka kikundi  chake kinachohusika  na   usimamizi wa  uzoaji taka na ukusanyaji wa ushuru wa Usafi majumbani na  Soko la Misungwi Mjini na kuzuia kikundi halali  kilichowekwa kisheria kukusanya na kufanya usafi wa soko hilo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halamshauri ya Wilaya ya Misungwi Bw, Benson Mihayo amesema kuwa Menejimenti kwa ujumla imepokea mapungufu yaliyobainishwa katika taarifa hiyo ya masoko na kwamba tayari  ameshaanza kuchukua hatua na kuweka mikakati ya kukusanya kikamilifu ushuru huo kwa mujibu wa sheria katika masoko ya Usagara, Misungwi, Nyashishi na masoko mengine na kuondoa mianya yote ya upotevu wa mapato na kuhakikisha kuwa mapendekezo yote 19 yaliyowasilishwa yatatekelezwa kikamilifu na kwa wakati.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe,Veronika Kessy(aliyesimama) wa tatu kushoto ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Misungwi Bw,Petro Sabato na anayefuata ni Kaimu Mkurugenzi Bw, Benson Mihayo akitoa maelekezo hayo juzi katika kikao cha tathmini na kupokea taarifa ya Maendeleo ya wa shughuli za masoko Wilayani Misungwi

Afisa wa TAKUKURU Wilaya ya Misungwi Bw,Erasto Maonyesho akiwasilisha taarifa ya Uchambuzi wa usimamizi na uendeshaji wa masoko katika kikao cha tathmini ya Maendeleo ya shughuli ya utekelezaji Wilayani Misungwi mapema wiki hii.

Baadhi ya Watumishi na wageni walikwa mbali mbali wakisikiliza kwa makini mjadala wa  kikao cha tathmini na maendeleo ya utekelezaji wa shughuli za masoko Wilayani Misungwi, kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri tarehe 9,Januari 2023.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.