• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DC Misungwi ashriki uchimbaji msingi na Wananchi ujenzi wa Sekondari mpya ya Wasichana Mwanagwa

Imewekwa : June 5th, 2022

Ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari ya wasichana Mwanangwa kupunguza utoro wa Wanafunzi Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe,Veronika Kessy amezindua uchimbaji wa msingi wa Shule ya Sekondari Maalum ya Wasichana Mwangwa iliyopo kata ya Mabuki Wilaya ya Misungwi amesema kuwa  ni hamasa kubwa  kwa jamii  kuendelea kushiriki katika miradi mbalimbali ya maendeleo.

Akizungumza na Wananchi wa Kata ya Mabuki amesema shule hiyo ambayo itagharimu Zaidi ya shilingi milioni 700,000,000/= itasaidia kupunguza utoro kwa wanafunzi shuleni na kuzingatia masomo yao na kuwa hamasa ya kujisomea, hata hivyoameongeza kuwa kutakuwa na awamu ya kwanza itakayoanza na majengo 4  ambayo yatagharimu shilingi milioni 457,000,000/=likiwemo bweni la wasichana,bwalo kwa ajili ya chakula na vyumba 4 vya madarasa pamoja na ofisi za Walimu.

Mhe. Veronika Kessy ameongeza kuwa majengo hayo yanatarajiwa kukamilika Mwezi wa tisa mwaka 2022,na shule hiyo itapokea wanafunzi wa kike kutoka sehemu mbalimbali ya Wilaya ya Misungwi watakao kuwa na vigezo vya kujiunga na shule hiyo vitakavyokuwa vimewekwa.

Katika Hafla hiyo Mhe.Veronika Kessy amewashukuru Wananchi kwa kujitokeza kwa wingi katika kushiriki uchimbaji wa msingi wa Shule  hiyo ya Sekondari Mwanagwa kwa kuokoa gharama za ujenzi katika hatua ya msingi ambapo fedha hiyo ingetumika kuchimba msingi badala yake itatumika kwenye matumizi mengine .Nakutoa wito kwa wananchi waendelee kujitokeza kuiunga mkono Serikali katika kushiriki shughuli za miradi ya maendeleo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Misungwi Bw Benson Mihayo ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita kwa kuleta fedha shilingi 475,000,000/=kwa awamu ya kwanza ambazo zinajengwa kupitia mpango  wa TASAF ambazo zitatumika kujenga shule ya Sekondari ya wasichana Mwanangwa kwa ajili ya kutatua tatizo la umbali na ushawishi kwa wanafunzi wanapotembea umbali mrefu wakati wa kwenda shule,na itasaidia wanafunzi kusoma kwa ufanisi na kufaulu vizuri katika mitihani yao.

Naye Afisa Elimu Sekondari Bi Diana Kuboja amesema Shule hiyo itasaidia kupunguza umbali kwa wanafunzi wa naoishi vijiji vya  mbali,ambapo kwa sasa wanafunzi wanatoka  zaidi kilomita ishirini kutoka kwenye makazi hadi eneo la shule  ya Sekondari Mawe matatu watafaidika na mradi huo. Sambamba hilo amesema kuwa Shule hiyo itakuwa una uwezo mkubwa  kubeba wanafunzi takribani wasiopungua mia nne.

Ameongeza kuwa Shule hiyo itaanza na madarasa manne ambayo yatabeba wanafunzi wasio pungua mia mbili na bweni moja  la wanafuzi litakalo chukua wanafunzi themanini.Pia shule ipo eneo sahihi kwa ajili kusaidia kupunguza umbali kwa wanafunzi wanaotoka katika kijiji cha Mwagagala na maeneo mengine.

Naye mkazi wa Kata ya Mabuki Bw.Peter Masalu amesema kuwa ujenzi wa Shule hiyo utasaidia kupunguza umbali kwa wanafunzi wanaotoka vijiji vya mbali ,pia itawasaidia wanafunzi kuwahi vipindi vya masomo vya asubuhi tofauti na sasa ambapo wanafunzi wengi wanachelewa vipindi  kutokana na umbali uliopo.

Mwenyeki wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Mhe, Kashinje Machibya akishiriki katika uchimbaji wa msingi Shule ya Sekondari ya Wasichana Mwanangwa.


Diwani wa Kata ya Misungwi Mhe, Muganyizi Ferouzi (katikati) akichimba msingi katika Shule ya Sekondari Mwanangwa akiwa na baadhi ya Wananchi waliojitokeza katika zoezi hilo wa Kata ya Mabuki.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.