• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DC Misungwi Akerwa na Awaonya Wanaume Wanaokatisha ndoto Kwa Watoto wa Kike

Imewekwa : September 11th, 2023

Serikali imesitisha jaribio la Mwanafunzi wa Kidato cha tano kuodheshwa kwa Mwanaume Askari Jeshi mara baada ya kurejeshwa kwa mahali ya Milioni mbili na Nusu zilizotolewa kwa Wazazi wake Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Tamko hilo limetolewa na Mkuu wa Wiaya ya Misungwi Mhe, Paulo Chacha katika kijiji cha Mamaye Kata ya Mamaye Wilayani Misungwi katika Familia ya Mwanafunzi  Anisia Pauline  Luchagula ambaye amenusurika kukatishwa ndoto zake za kuendelea na  masomo ya kidato cha Tano  katika Sekondari ya Bukongo Wilayani Ukerewe.

Mhe, Chacha amekemea vikali kitendo cha wazazi kukatisha ndoto na malengo ya watoto wao kimasomo  jambo ambalo halikubaliki na linawanyima haki zao za msingi kama vile kupata elimu kwa ajili ya maisha yao na taifa kwa ujumla,pia ametoa mahitaji ya msingi ya kujikimu kwa mwanafunzi huyo pamoja na fedha taslimu shilingi 300,000/=.

“Baba mtu mzima mwanaume anamwita mtoto wa kike Mchumba akamatwe kabla hajaenda mbele, baadala amwite Mwanangu, mdogo wangu, lakini anajisikia fahari kumwita mchumba katoto kadogo tu ”   Ameonya Mhe, Mkuu wa Wilaya, Paulo Chacha.

Mhe, Paul Chacha amesema ukaribu na Wananchi Wilayani humo umeweka urahisi wa kupokea taarifa hizo na kusema  hatua zitachukuliwa Kwa mtumishi huyo na hatimaye kuagiza kufikishwa salama  mwanafunzi huyo kufika Wilaya ya ukerewe katika shule aliofaulu  kuendelea na masomo  yake.

Mkuu wa Wilaya huyo ametoa Rai kwa wazazi kuhakikisha wanatimiza majukumu yao na kuacha mara moja vitendo vya kuwaodhesha watoto  wakiwa masomoni ni jambo ambalo ni kinyume na Sheria , na taratibu za nchi na ukatili dhidi ya watoto.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Misungwi, Bi Aziza Mangu amesema kitendo kilichotokea cha kutaka kukatishwa masomo hakikubaliki katika jamii hivyo kupitia jitihada za uongozi wa Wilaya hatutarajii tena kitendo kama hicho kutokea kwa wanafunzi wengine na kuiomba jamii kubadilika.

Afisa Elimu wa Kata ya Igokelo Wilaya ya Misungwi Bw. Hashimu Zaidi akimwakilisha Afisa Elimu Sekondari amesema kwamba mwanafunzi huyo amekuwa na maendeleo mazuri na ufaulu wa dalaja la pili katika mchepuo wa sayansi katika masomo ya Kemia,Biolojia na Jiografia (CBG) na ni miongoni mwa Watoto 6 waliofanya vizuri hivyo kitendo hiki hakivumiliki na hatutokubali  anatakiwa kuendelea na masomo yake ya kidato cha tano bila kukatishwa ndoto zake .

Wakati huo huo, Baba Mzazi wa Alisia Bw. Pauline Luchagula ameomba radhi kwa kitendo cha kutaka kumuodhesha binti kinyume na sheria na kanuni za nchi hivyo amekiri kutokutokea tena kwa kitendo hicho na kutoa wito kwa familia zingine zijifunze kupitia familia yake kwa watoto wao na iwe fundisho kwa familia zingine za hapo kijijini na ndugu na jamaa.

Naye, Mama Mzazi wa binti hyuo Bi. Maria Ng'aya Mama mzazi wa mwanafunzi huyo alikiri kutokea kitendo hicho ambapo amesema jambo hilo walilifanya kwa kutotegemea na hawakulazimishwa bali walifanya bila kukusudia na kuushukuru uongozi kwa kuingilia  suala hili na amesema mwanaye sasa aende akasome na hatorudia tena.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe,Paulo Chacha akimwaaga Mwanafunzi Bi Anisia Pauline  Luchagula  chini ya usimamizi mkali wakati akielekea Wilayani Ukerewe kwa ajili ya Masomo yake hivi karibuni,ambapo DC alimkabidhi Fedha taslimu shilingi 300,000/= pamoja na mahitaji mengine ya kujikimu.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.