• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DC Misungwi akagua Miradi vijijini, apongeza Wananchi kwa kujenga Madarasa matano na Nyumba tatu za Walimu Sumbugu

Imewekwa : January 31st, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda apongeza Wananchi wa Kata ya Sumbugu kwa kukamilisha ujenzi wa vyumba vitano vya madarasa walivyojenga kwa  nguvu na michango yao na kuwataka kuhakikisha watoto wao wanasoma kwa bidii na kufuta ufaulu wa daraja sifuri katika mtihani wa kidato cha nne mwaka huu 2020.

Pongezi hizo zimetolewa katika kikao cha Viongozi wa Kata  ya Sumbugu na Mkuu wa Wilaya ya Misungwi wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua miradi pamoja na shughuli za maendeleo zinazotekelezwa katika Kata na vijiji vya Halmashauri ya Wilaya ya Misugwi, ambapo katika Shule ya Sekondari Sumbugu Madarasa hayo yamejengwa  na Wananchi ili kuwezesha kusoma Wanafunzi 247 waliochaguliwa  kuanza kidato cha kwanza mwaka huu 2020 katika Shule ya Sekondari Sumbugu.

Mkuu wa Wilaya,  Juma Sweda, amesema kwamba Wananchi hao wamejitahidi sana kujenga madarasa kwa nguvu zao na wameonyesha umoja na ushirikiano mkubwa hatimaye wamefanikiwa kujenga vyumba vitano kati ya vyumba saba vinavyotakiwa kulingana na mahitaji ya Wanafunzi 748 wa shule hiyo, ambapo ameahidi kuwachangia kwa kukamilisha ujenzi wa sakafu katika darasa moja.

 Akizungumza na Viongozi wa Kata hiyo amewasihi na kuwaeleza umuhimu wa elimu kwa watoto na kwa maendeleo yao na taifa kwa ujumla, na kuwataka kuhakikisha wanaondoa ufaulu wa daraja sifuri katika mtihani wa Kidato cha nne mwaka huu,  “ Zero hapana katika Sekondari ya Sumbugu, alisema kwa msisitizo Juma Sweda.”

Amewataka Walimu shuleni hapo kufundisha kwa bidii zaidi na kukamilisha mada zote mapema ili kuwapa fursa wanafunzi kupata mazoezi ya kutosha ya maandalizi ya Mtihani, na amewaonya Wananchi waliozoea na watakaothubutu kuwapa mimba watoto wa shule na kueleza kuwa watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria za nchi.

Awali, katika ziara yake Mkuu wa Wilaya huyo amekagua na kuridhishwa na ujenzi wa Nyumba tatu za Walimu zilizojengwa na kukamilika katika Shule ya msingi Sumbugu ambazo pia zimejengwa  kwa nguvu na michango ya Wananchi wa Kijiji cha Sumbugu, na kuwaomba Wananchi wa maeneo ya vijiji vingine kuiga mfano huo wa ushirikiano na moyo wa kujituma katika maendeleo kwa lengo la kuboresha na kukuza sekta ya elimu nchini.

Juma Sweda, amewasihi Walimu wa shule hiyo kuwajibika kikamilifu kwa kuzingatia kanuni taratibu na sheria za utumishi wa umma ikiwemo kuwahi kazini  na kufundisha kwa bidii na kuwaonya Walimu wenye tabia ya uchelewaji kazini, vitendo ambavyo vinazorotesha maendeleo  ya taaluma kwa Wanafunzi na kusababisha kudorola kwa ufaulu katika mitihani yao ya kumaliza elimu ya msingi.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, amekagua na kuona maendeleo katika sekta ya Afya, ambapo katika Zahanati ya Sumbugu amebaini kuwepo kwa  utaratibu mbovu wa utunzaji wa kumbukumbu na takwimu za utoaji wa madawa katika stoo ya dawa na kutoa maelekezo kwa TAKUKURU kufuatilia taratibu hizo na kutoa taaarifa mapema.    

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda (kushoto) akikagua leja ya dawa kuona namna utaratibu wa utoaji dawa katika stoo kwenda kwa Wagonjwa unavyofanywa na utunzaji wa kumbukumbu na akipewa maelezo kuhusu utaraibu kutoka kwa Muuguzi wa Zahanati ya Sumbugu, (katikati ni) Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Sumbugu Ezrom Mwanga akishuhudia zoezi la ukaguzi huo.

Jengo la vyumba vya Madarasa matano vilivyojengwa na Wananchi katika Sekondari ya Kata ya Sumbugu, Madarasa haya yanatarajiwa kuanza kutumiwa na Wanafunzi kuanzia wiki ijayo 

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.