• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DC Misungwi ahimiza Madiwani na Watendaji kuongeza kasi ya ukusanyaji Mapato mwaka 2024/2025

Imewekwa : August 1st, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe, Johari Samizi aagiza Baraza la Madiwani na Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kuhakikisha wanasimamia kikamilifu ukusanyaji wa Mapato ya Ndani shilingi Bilioni 4,704,013,000/=kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Mhe, Johari Samizi amesema kwamba hakuna nchi wala Halmashauri inayoweza kuendeshwa bila kuhakikisha ukusanyaji wa mapato unaimarika , na siyo tu kukusanya na kuhakikisha kwamba yanatumika ipasavyo, na amesisitiza Idara zote zinazohusika na ukusanyaji wa mapato kuweka mikakati madhubuti, kwamba tumeanza mwaka mpya wa Serikali, hivyo idara zinazohusika zikusanye mapato kwa uaminifu na kwa uadilifu na mapato haya yakatumike kuwaletea maendeleo Wananchi kama ambavyo Serikali imekusudia.

“Amesema hatarajii kwa mwaka huu wa fedha 2024/2025 kuwa mkusanya mapato kukaa na fedha ya Serikali bila kupeleka benki zaidi ya masaa ishirini na nne (24) endapo itatokea hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake” Alisisitiza DC Johari Samizi.

Mhe,Johari Samizi amewawasistiza Viongozi na Watendaji wawe na vipaumbele vya kufanya mabadiliko ya vifungu vya matumizi katika shughuri za maendeleo tu na sivinginevyo na kuendelea kutekeleza miradi kikamilifu pia amewataka Wananchi kuachana na shughuli zote za kibinanadamu katika vyanzo vya maji na maeneo tengefu ili kuimarisha usalama wa mazingira na kuepuka mabadiriko ya tabia ya nchi kwa ujumla na kusisitiza matumizi ya Nishati mbadala ya kupikia.

Mhe, Mkuu wa Wilaya huyo amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kufanya mabadiliko makubwa kuliko awamu zote na kujenga na kukamilisha miradi mingi na mikubwa katika Wilaya ya Misungwi ikiwemo Chuo cha Uhasibu TIA Usagara na kueleza kuwa kufikia mwezi Disemba 2024 miradi yote itakuwa imekamilika ikiwemo Daraja la JPM la Kigongo –Busisi pamoja na kuwataka Wananchi kushiriki katika Uchaguzi wa Serikari za mitaa mwaka 2024 kwa kuboresha Daftari la kudumu la Wapiga kura na kupata haki ya kumchagua kiongozi anayempenda kwa maendeleo ya taifa.

Akizungumza wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani katika ukumbi wa Halmashauri Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Mhe, Machibya ameeleza kwamba Baraza la Madiwani halitokuwa tayari kumvumilia Kiongozi ama mfanyabiashara yoyote atakaye sababisha na kuleta ukwamishaji katika suala la Ukusanyaji wa Mapato kwa kuzingatia kipaumbele cha Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ni Mapato, Mapato na Mapato ili kuweza kupeleka asilimai 40 za mapato katika kutekeleza miradi ya  vijijini.

Mhe, Machibya amesema kwamba Baraza la Madiwani lina wajibu wa kusimamia mapato ya ndani kwa  bidii  kwa maslahi mapana ya Wananchi na kuhakikisha kutokutoa mwanya wa upotevu wa mapato kwa namna yeyote ile na kuwataka Watendaji wa Kata kuendelea kusimamia na kutumia kikamilifu fedha za Miradi ya Maendeleo ili ziendane na thamani ya fedha katika miradi husika.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Misungwi Mhe, Emmanuel Masangwa ameipongeza Halmashauri kupitia Madiwani,Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na Watendaji wote kuhakikisha wanasimamia fedha za Miradi ya maendeleo kwa umakini mkubwa ili kuwaletea maendeleo Wananchi na kuwaomba Viongozi pamaoja na Watendaji kuongeza ushirikiano katika kuwaletea Wananchi maendeleo ya dhati.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bw.Addo Missama amemshukuru Mhe, Rais kwa kumteua na kuwaomba Madiwani, Watendaji kumpatia ushirikiano wa kutosha katika kutekeleza shughuli za Serikali na kutimiza malengo yaliyowekwa na kuahidi kufanya kazi kwa mujibu wa taratibu na sheria ili kuweza kuwaletea maendeleo Wananchiwa Wilaya ya Misungwi.



Baadhi ya Wajumbe wa Baraza la Madiwani Misungwi wakiwa katika kikao Cha Baraza robo ya Nje Mwezi Julai 2024 

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.