• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DC Misungwi afungua bweni la kisasa lenye thamani ya Milioni 120 Sekondari ya Misungwi

Imewekwa : November 30th, 2020

Mkuu wa WIlaya ya Misungwi, Juma Sweda azindua na kufungua Bweni la Wasichana lililogharimu kiasi cha shilingi Milioni 120 katika Shule ya Sekondari Misungwi, Mkoani Mwanza  

Akizungumza katika hafla ya uwekaji wa Jiwe la ufunguzi wa bweni hilo Mkuu wa Wilaya ya Misungwi,  Juma Sweda amesema na kupongeza uongozi wa Sekondari hiyo kupitia kwa Mkuu wa Shule hiyo ambaye amekuwa mstari wa mbele na ameonyesha kwamba ni mchapakazi na mwenye moyo wa kupenda maendeleo ya jamii na siyo mtu wa kufanya mambo binafsi na kujinufaisha ndio sababu amefanikiwa na kukamilisha ujenzi wa bweni baada ya kubana matumizi mbalimbali ya shule ikiwemo Chakula.

Ameeleza kwamba bweni hilo litaleta na kuongeza chachu ya kusoma kwa Wanafunzi na kuwataka wanapomaliza wasisahau Wilaya ya Misungwi na kuendelea kuikumbuka daima katika maisha yao, hivyo jukumu kubwa sasa baada ya kukamilika kwa bweni ni kusoma kwa bidii na kuongeza ufaulu katika Mitihani.

“ Hili ni bweni ambalo  kimsingi  ni bweni la mfano unaweza ukaangalia hata Mkoa wa Mwanza bweni kama hili unaweza usilpate ni bweni ambalo lina facilities zote  na ni bweni la kisasa sana ” Alisema  kwa kusisitiza Juma Sweda.

Juma Sweda amewahakikishia Wanafunzi hao wa Kidato cha tano na sita kwamba Serikali itaendelea kuboresha miundombinu na mazingira yao na kuwawezesha  kusoma vizuri  ili kuongeza ufaulu zaidi na kuwaomba  kulitumia vizuri  bweni hilo zuri ambalo lina mahitaji yote yanayopaswa kuwepo bwenini na ni la kisasa zaidi.

Naye Mkuu wa Shule ya Sekondari Misungwi, Ananius Mbandwa ameeleza katika taarifa ya mafanikio ya shule hiyo kwamba  Shule hiyo imeanzishwa mwak 1994 na kufanikiwa kunza Kidato cha tano mwaka 2016 katika mchepuo wa EGM na CBG

Akifafanua zaidi  katika suala la ujenzi wa bweni hilo uliogharimu kiasi cha shilingi Milioni 120 na laki tano hadi kukamilika ambapo fedha zilizotumika ni fedha shilingi Milioni 40 ya mapato ya ndani ya Sekondari hiyo ambayo imetokana na bakaa  na bana matumizi ya fedha ya Chakula kwa Wanafunzi na fedha shilingi Milioni 60 ambayo ni kutoka Serikali kuu kupitia Wiazra ya Elimu

Bw, Mbandwa ameeleza  na kufafanua kwamba bweni hilo lina uwezo wa kukaa  vitanda 40 vya aina ya Deka kwa Wanafunzi zaidi ya 80 ambapo kwa sasa litatumiwa na Wanafunzi zaidi ya 80 ambao ni 50 wa Kidato cha sita na 30 wa Kidato cha tano waliopo kwa mwaka huu 2020/2021

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Kisena Mabuba amewapongeza Viongozi wa Shule ya Sekondari Misungwi kwa ushirikiano na juhudi za makusudi za  kuleta mabadiliko  ya elimu wanazoendelea kuzifanya hususani katika matokeo ya Wanafunzi wa Kidato cha Nne na Sita kwa hakika Wanafunzi hawa wanaendelea kupindua meza kibabe tu.


Mwonekano wa bweni la kisasa la Wasichana lilojengwa na kukamilika katika Shule ya Sekondari Misungwi linaloweza kubeba Wanafunzi 80 wa Kidato cha tano na sita , bweni hilo limegharimu shilingi Milioni 120 tu fedha za Serkali.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda (katikati) akikata utepe kuashairia ufunguzi rasmi wa Jengo la bweni hilo akiwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Kisena Mabuba wa kwanza kushoto akifuatiwa na Katibu Tawala Wilaya ya Misungwi, Petro Sabatto na Afisa Elimu Sekondari Diana Kuboja pamoja na Walimu na Wanafunzi wwa Kidato cha tano na sita.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda akiangalia na kukagua eneo la kunawa mikono katia moja wapo ya bafu ndani ya Jengo la bweni la Wanafunzi katika Sekondari ya Misungwi.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.