• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DC Misungwi acharuka,Aagiza msako wa kukamata Wazazi wasiopeleka watoto Shule

Imewekwa : January 23rd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Paulo Chacha amewagiza Viongozi wa Tarafa, Kata na Vijiji kuwasaka na kuwakamata Wazazi ambao hawajawapeleka watoto kuripoti shule kuanza masomo ya kidato cha kwanza mwaka 2023 Wilayani Misungwi.

Mhe, Paulo Chacha ametoa agizo hilo mapema leo katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya ya Misungwi mara baada ya kubaini na kuona hali halisi ya watoto ambao wamesharipoti na kuanza masomo ya Kidato cha kwanza tangu tarehe 8, Januari 2024 na kutoridhishwa na mahudhurio ya Wanafunzi wa Kidato cha kwanza.

Amewataka Maafisa Tarafa, Watendaji wa Kata na Vijiji kwa kushirikiana na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji kuwabaini Wazazi na Walezi wa watoto wote ambao mpaka sasa  hawajaanza masomo na kuwapeleka Kituo cha Polisi kwa ajili ya kuwachukulia hatua za kisheria kwa kosa la kuwanyima watoto haki ya msingi ya kupata elimu ya Sekondari ambapo amekea suala la Wazazi kiuwaozesha watoto na wengine kuwapeleka kufanya kazi za kilimo na mifugo pamoja na uchimbaji wa madini.

Aidha, agizo hilo pia linahusu Wazazi wenye watoto ambao hawakufanya Mtihani wa Kidato cha pili Wanafunzi wapatao 630 kutoka katika shule zote 37 za Wilaya ya Misungwi pamoja na wanafunzi wa Kidato cha Nne mwaka 2023 wote kwa pamoja watafutwe na kurejeshwa shule kwa ajili ya kuendelea na masomo na kufanya mitihani husika.

Mkuu wa Wilaya huyo ameipongeza rasimu ya Bajeti ya Halmashauri na kuwataka Watendaji kujipanga vizuri kutekeleza miradi kwa uadilifu na kuikamilisha kwa wakati na ubora na kwa viwango pamoja na kuweka jitihada kubwa katika ukusanyaji wa mapato ya ndani na kufikia malengo yaliyokusudiwa na kuleta tija katika jamii.

Awali akiwasilisha rasimu ya Bajeti  katika kikao hicho cha kupitia mapendekezo  ya rasimu ya Bajeti ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2024/2025 kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bi. Peniel Titus amesema kuwa Halmashauri inatarajia kukusanya na kutumia kiasi cha shilingi Bilioni 51.4 kwa ajili ya utekelezaji wa wa shughuli mbalimbali za Halmashauri ikwa ni pamoja na malipo ya Mishahara ya Watumishi kiasi cha shilingi Bilioni 36,792,448,000, fedha za Ruzuku ya uendeshaji wa Ofisi (OC) kiasi cha shilingi 1,359,841,000, na katika kutekeleza miradi ya maendeleo kwa shilingi Bilioni 8,636,386,000.

Afisa Mipango huyo alieleza kwamba kwa upande wa  na Mapato ya ndani Halmashauri imekisia kukusanya na kutumia kiasi cha shilingi 4,677,820,361 kutoka vyanzo  vya mapato ya ndani ambapo kati ya fedha hizo Bilioni 3,946,152,361 ni Mapato halisi na Shilingi Milioni 31,668,000 ni Mapato Lindwa.

Bi. Peniel Titus ameongeza na kufafanua kwamba makadirio ya Mapato ya ndani kwa Mwaka 2024/202425 yameongezeka kwa asilimia 4.15 kutoka Shilingi Bilioni 4,483,664,000.04 mwaka 2023/24 hadi shilingi Bilioni  4,677,820,361.3 kwa kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa matumizi ya mfumo wa kielektoniki wa ukusanyaji wa mapato ikiwa na kuhakikisha fedha zote zinazokusanywa zinawekwa Benki kwa wakati, kuongezeka kwa watumiaji wa madini ujenzi hususani mchanga na mawe iliyopelekea kuongezeka kwa mapato ya madini ya ujenzi pamoja na kuongezeka kwa idadi ya viwanda na makampuni yaliyopelekea kupanda kwa ushuru wa huduma.

Kwa upande wake  Meneja wa Wakala wa Maji safi na taka Vijijini (RUWASA) Wilaya ya Misungwi Mhandisi Bw. Marwa Kisibo ameeleza kuwa kiasi cha fedha kilichotengwa katika Bajeti 2023/2024  ni Shilingi Bilioni 1,986,416,209.67 kitanufaisha zaidi ya wakazi 173,031 katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ambapo baadhi ya  hiyo ni Mradi ya  Mabuki,Ilujamate –Buhingo,Kigongo,Ukiliguru,Koromije hadi Usagara,Igongwa,Nguge,Mabale Mbarika,Kijima hadi Isakamawe,Ngaya- Matale.

Sambamba na hayo ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuendelea kutenga fedha kwa ajili Miradi mbalimbali ya maendeleo kwa manufaa ya Wananchi na kuahidi kusimamia kikamilifu kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ili miradi hiyo iweze kuleta tija kwa wananchi na Taifa kwa ujumla.

Naye Katibu wa CCM Wilaya ya Misungwi Bw. Mwita  Nyarukururu ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa ushirikiano mzuri na  kusimamia kikamilifu pamoja na  juhudi zinazofanyika kuhakikisha Mapato ya ndani yanaongezeka,na kuwataka Watendaji  kuendelea kusimamia ukusanyaji wa mapato vizuri pamoja na  mchakato wa  kuwa na POS katika ngazi za Vijiji ili kuokoa mapato yanayopotea katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi na kwamba CCM itaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali ya awamu ya sita.

Mkuregenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bw,Joseph Mafuru aliyesimama kwa mbali akitoa ufafanuzi kwa wajumbe juu ya mapendekezo ya mpango wa Bajeti ya Halmashauri kwa Mwaka wa fedha 2024/2025 katika Ukumbi wa Halmashauri ya Misungwi.

Katibu wa CCM Wilaya ya Misungwi Bw, Mwita Nyarukururu kushoto akizungumza katika  Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Wilaya kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri kwa ajili ya kupitia  Bajeti ya Mapato na Matumizi ya Halmashauri ya Mwaka 2024/2025.wa pili kushoto ni  Katibu Tawala Wilaya Bw, Abdi Makange akifuatiwa na Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe,Paul Chacha (kulia) pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Misungwi Bw,Joseph Mafuru wa kwanza (kulia).

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.