• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DC Misungwi awataka Wawekezaji nchini kuwekeza Viwanda Misungwi, hekari 74 za Viwanja zatengwa

Imewekwa : May 14th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mkoani Mwanza, Juma Sweda atoa Wito kwa  Wawekezaji nchini  kuwekeza Viwanda katika maeneo ya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa lengo la  kutoa ajira na kukuza uchumi wa Wilaya ya Misungwi na taifa kwa ujumla.

Akizungumza na Wanahabari mapema jana katika ziara ya Kamati ya Ulinzi na Usalama alipotembelea  na kukagua Viwanda vya Sayona Steel LTD na Kiwanda cha Mkate cha  Royal Supermaket  vya Wilayani Misungwi, Juma Sweda amewataka wenye Viwanda kuendelea kuzalisha kwa wingi na kuwaomba Wananchi kutumia bidhaa zitokanazo na Viwanda vya ndani na hatimaye Soko la ndani litaendelea kuimarika zaidi.

Juma Sweda ametoa Wito kwa Wawekezaji na wenye Viwanda kuja kuwekeza katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ambapo tayari wametenga Viwanja na eneo la Mitindo lenye Hekari 74  ambazo zinatolewa bure kwa Wawekezaji kwa ajili ya kujenga Viwanda vya kuzalisha bidhaa na vifaa vya aina mbalimbali na kuweza kutoa ajira kwa Wananchi wa Wilaya ya Misungwi.

Kwa upande wake Meneja Uzalishaji na Masoko wa Kiwanda cha Sayona Steel LTD cha Wilayani Misungwi, Sunny Naker amewaomba Wafanyabiashara na Wananchi wa Wilaya ya Misungwi na Watanzania wote kuvitumia bidhaa zinazozalishwa katika Kiwanda hicho zikiwemo masufuria,Steel wire na Nondo ambazo zinapatikana kwa wingi  Kiwandani hapo.

Amesema kwamba biashara kwa muda sasa imesuasua kutokana na changamoto za mvua zilizokuwa zinanyesha na kusababisha kupungua kwa Wateja wa ndani na Soko la nje, na kueleza kwamba matarajio yao ni kuanza kuuza bidhaa za Nondo hivi karibuni baada ya Wananchi kuanza shughuli za ujenzi na kwamba wanatarajia kurejea katika uzalishaji wa Nondo na bidhaa zingine za ujenzi kama kawaida.

Katika ziara hiyo wameweza kukagua pia shughuli za ujenzi wa Kiwanda cha Mkate cha Royal Supermarket kinachojengwa maeneo ya Nyashishi Wilayani Misungwi ambapo ujenzi unaendelea vizuri na matarajio ya kukamilisha ni mapema mwezi Septemba mwaka huu baada ya kusimika mitambo ya uzalishaji wa bidhaa ya Mkate.

Mkuu wa Wialaya ya Misungwi, Juma Sweda (katikati) akiangalia Masufuria ambayo ni moja ya bidhaa zinazozalishwa na Kiwanda cha Sayona Steel LTD kilichopo maeneo ya Nyanghomango Wilayani Misungwi, (wa kwanza kulia ni Meneja Uzalishaji na Masoko wa Kiwanda hicho, Sunny Naker akifuatiwa baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya walioambatana na Mkuu wa Wilaya huyo katika ziara hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda (kushoto) akikagua maeneo na kuona shughuli za uzalishaji wa bidhaa mbalimbali zinazozalishwa katika Kiwanda cha Sayona Steel LTD kinachozalisha bidhaa ya Sufuria, Steel wire  Nondo na bidhaa za zingine zinazotumika katika ujenzi,  

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.