• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DC awataka Wahitimu Jeshi la Akiba kujiunga katika Vikundi ili kuongeza kipato Wilayani Misungwi

Imewekwa : October 31st, 2021

Wahitimu wa Jeshi la Akiba waaswa kuchangamkia Ajira kwa kujiunga katika vikundi mbalimbali vya ujasiriamali Wilayani Misungwi, Mkoani Mwanza,.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Misungwi  Mhe.Veronica Kessy wakati akifunga mafunzo ya Jeshi la Akiba katika Viwanja vya Shule ya Msingi Misungwi  Mwanakanenge Wilayani humo  mwishoni mwa wiki,  na kuwataka kuchangamkia fursa kwa kuwa katika Vikundi mbalimbali kwa lengo la kujipatia kipato na kukuza uchumi wao binafsi, pia amewaasa wahitimu hao kuendelea kudumisha amani, utulivu na mshikamano uliopo na  kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa vitendo.

Akizungumza na Wananchi Bi. Veronika Kessy amewataka wahitimu hao kuwa mfano wa kuigwa katika jamii kwa kuwa waadilifu,kujituma na  kuwa na moyo wa uzalendo katika kujenga nchi yao, sambamba na hilo amewataka kuanzisha vikundi na hasa vikundi vya afya na usafi wa mazingira  na kuwa wajasiriamali wanaotambulika ili kuweza kujipatia mikopo ya Srikali kutoka Halmashauri  itakayowawezesha kujikwamua na tatizo la ajira na kukuza uchumi wa familia zao..

Mkuu wa Wilaya huyo ameongeza kuwa Wananchi wa Misungwi kwa sasa wamehamasika na wanapaswa kuendelea kujitokeza kwenda kupata Chanjo ya UVIKO 19 ambapo Chanjo hiyo inasaidia kuongeza Kinga ya mwili na kupunguza makli ya ugonjwa pamoja na Vifo 

Amewataka Wananchi kuendelea kuchukua tahadhari juu ya maambikizi ya Ugonjwa  wa Corona  na kuendelea kujikinga kwa kufuata na kuzingatia ushauri wa Wataalam wa Afya nchini kiwa ni pamoja na kuvaa barakoa, kuepuka misongamano, kunawa mikono kwa maji tiririka mara kwa mara pamoja na kufanya mazoezi.

Aidha, amesema kuwa Wananchi wanatakiwa kujitokeza kuhesabiwa katika zoezi la Sensa hapo mwakani 2021,pindi muda utakapofika ili kurahisha zoezi hilo kwani lina manufaa makubwa kwa wananchi na hata kwa taifa kwa ujumla katika kupanga mipango yake ya maendeleo.

Kwa upande wake Mshauri wa Jeshi la Akiba Wilayani  Misungwi Meja Matemi amesema katika mafunzo hayo ambapo jumla ya  Wahitimu 52 wamemaliza  mafunzo hayo wakiwemo vijana wa kiume 39 na  vijana wa kike 13, na kueleza na kuwataka Wahitimu hao kuwashukuru wazazi/walezi  kuwaruhusu vijana wao kushiriki mafunzo na kuweza kuhitimu.

Wakati huo huo Meja Mateni amewataka wahitimu hao kuwa  waadilifu na wazalendo katika kutumikia taifa lao kwa kujitoa katika shughuli za kiuchumi na kijamii pamoja kuwa mstari wa mbele kusaidia taifa katika majanga na matatizo mengine yanapotokea.

Baadhi ya washiriki waliohitimu  wamefarijika na mafunzo hayo na yamewajengea uwezo mkubwa wa  kukabiliana na changamoto za kimaisha ambazo zinawakabili na zinazoweza kujitokeza katika shughuli zao za kila siku.

Mmoja wa Wahitimu wa Jeshi la Akiba, Bi. Prisca Augustine amewashauri vijana wenzake ambao bado hawajajiunga na Jeshi hilo kwamba wajiandae  kufanya hivyo kwa manufaa yao wenyewe  na taifa kwa ujumla kwani wanaweza kujipatia ajira kwa kuajiriwa katika makampuni mbalimbali pamoja na kujiajiri wao wenyewe kupitia fursa za vikundi vya ujasiriamali

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.