• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DC aagiza Madiwani na Watendaji kusimamia kikamilifu upatikanaji wa chakula Shule za Msingi na Sekondari

Imewekwa : May 15th, 2023

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe, Paulo Chacha ahimiza Wahe.Madiwani na Watendaji wa Kata na Vijiji kuhakikisha wanasimamia upatikanaji wa chakula katika Shule za Sekondari na Msingi Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Wito ulitolewa mwishoni mwa wiki wakati wa Mkutano wa wadau wa Elimu uliofanyika katika ukumbi wa MGS Misungwi ambapo Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Paulo Chacha ambao ulilenga kujadili masuala ya uboreshaji wa Sekta ya Elimu sambamba na utoaji wa zawadi kwa shule za Msingi na Sekondari zilizofaya vizuri na zilizofanya vibaya pamoja na Walimu waliofanya vizuri katika Shule za Sekondari na Msingi.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi  Mhe, Paulo Chacha aliwataka Wahe,Madiwani,Watendaji wa Kata na Vijiji kuhakikisha wa wanasimamia kikamilifu zoezi la kukusanya chakula cha kutosha katika maeneo ya Kaya za Wananchi hasa katika kipindi cha mavuno na kuhakikisha chakula kinapatikana cha kutosha  mashuleni kwa ajili ya wanafunzi ili kuinua kiwango cha ufaulu kwa Shule zote za Msingi na Sekondari.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bw.Benson Mihayo alieleza kuwa mbali na Walimu hao kupewa zawadi fedha taslimu na vyeti pia Halmashauri imetoa viwanja kwa Watumishi hao kwa bei nafuu ambapo wanaweza kulipia kidogo kidogo na kupata  kiwanja chenye ukubwa wa Mita za mraba 800 kwa thamani ya shilingi Milioni moja na laki sita kama motisha.

Kwa upande Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza Bw.Martine Nkwabi aliekeza kwa Maafisa  elimu Kata na Watendaji wa Kata na vijijini kuhakikisha wanasimamia kikamilifu na kuondoa utoro kwa wanafunzi kwa Shule zote za Msingi na Sekondari, wakati huo huo  aliwataka kusimamia nidhamu mashuleni kwa Shule za msingi wahakikishe wanafunzi wanajua Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK).

Aidha, amesisitiza utoaji wa adhabu kwa wanafunzi uzingatie sheria na kanuni ili kuepusha madhara ambayo yanaweza kujitokeza kwa mwanafunzi pamoja na kuzingatia ufundishaji mzuri unaozingatia lugha za ustaha, haiba kwa mwalimu na kuheshimu ratiba za masomo.

Afisa Ustawi Mwandamizi kutoka Mkoa wa Mwanza Bi.Rehema alieleza na kufafanua kuwa suala la uadilifu katika jamii nzima ni muhimu na nilazima kuzingatiwa ili kutengeneza kizazi bora cha sasa na kijacho ambapo aliwaomba Wadau mbalimbali wa elimu kutoa ushirikiano endapo wataona kuna viashiria vya uvunjifu wa maadili kwa jamii zinazotunguka ikiwa ubakaji na ulawiti hasa kwa watoto.

Naye Afisa Elimu wa Sekondari Wilaya ya Misungwi Bi.Diana Kuboja alisema wataendelea kusimamia kikamilifu taaluma pamja na nidhamu mashuleni kwa Shule zote za Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ili kukuza ufaulu na Kuondoa ziro kwa Shule zile ambazo zimefanya vibaya,na kwa kuwapa Walimu motisha chanya kwa wale wanaofanya vizuri na zoezi hilo litakuwa endelevu.

Mwalimu Diana Joseph ambaye ni Mwalimu Mkuu wa Shule ya Exodus Primary school ambayo ni shule binafsi ameishukuru Serikali kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa kutambua juhudi za walimu kwa kutoa zawadi mbalimbali ikiwemo fedha taslimu pamoja na vyeti na zoezi hilo limewapa hamasa katika kuinua  na kuboresha kiwango cha elimu.

Kwaya ya Walimu wa Misungwi ikitumbuiza katika Mkutano wa Wadau wa Elimu katika ukumbi wa MGS wiki hii ambapo wadau mbalimbali walihudhuria Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe,Paulo Chacha.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe, Paulo Chacha  akimkabidhi zawadi ya Cheti cha pongezi Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bw.Benson Mihayo wakati wa Mkutano wa Wadau wa Elimu katika ukumbi wa MGS mapema wiki hii.

Afisa Elimu Mkoa wa Mwanza Bw.Martine Nkwabi kushoto akishuhudia Walimu wakikabidhiana kinyago kwa Shule iliyofanya vibaya katika matokeo ya Mitihani 2022.kama motisha hasi kwa Walimu hao.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.