• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DAS Misungwi awataka Vijana kutumia Pikipiki kwa malengo kusudiwa na kurejesha Mikopo kwa wakati

Imewekwa : February 1st, 2023

Katibu Tawala Wilaya ya Misungwi Bw, Petro Sabatto awataka Vijana wana kikundi cha Vijana kazi Kata ya Bulemeji  kuvilinda na kuvitumia vizuri vyombo vya usafiri wa Pikipiki  walizokepeshwa na Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi  zenye thamani ya shilingi milioni 26 Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza..

Akizungumza katika ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi katika Hfla ya makabidhiano ya pikipiki Katibu Tawala Wilaya ya Msungwi Bw, Petro Sabatto kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe, Matiko Paul Chacha amesema Halmashauri zihakikishe zinanatenga fedha asilimia 10 kwa ajili ya kuwakopesha vikundi mbalimbali ikiwemo  watu wenye ulemavu fedha hizo ambazo  hutolewa na kurejeshwa  bila riba.

Bw, Sabatto amesema na kuwaelekeza Vijana hao kuvilinda na kuvitumia vizuri vyombo vya usafiri wa Pikipiki  kwa matumizi yaliyokusudiwa ili waweze kuwapa manufaa ya kiuchumi na kuinua kipato chao pamoja na kurejesha mikopo kwa wakati na kuruhusu wengine kukopa kwa ajili ya kunua uchumi wa mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla.

“Na Misungwi tunaenda vizuri na ninyi mkawe mabalozi wazuri kwa vijana wengine waweze kujiunga  katika vikundi kupitia elimu inayoendelea kutolewa na Idara ya Maendeleo ya Jamii.” Alisisitiza Bw. Sabatto.

Akiwasilisha taarifa ya makabidhiano ya pikipiki hizo Kaimu Afisa  Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Misungwi, Bi.Juliana Mwongerezi amesema kuwa mradi huo umegharimu jumla ya shilingi milioni 26 ambazo ni mkopo kutoka Halmashauri ambao umetolewa kupitia asilimia 4 ya fedha za mapato ya ndani kwa robo ya pili  kuanzia mwezi Oktoba hadi Disemba 2022.

Aidha Bi.Mwogerezi ameongeza kuwa mbali na kukundi cha Vijana kazi kupata Mkopo isiokuwa na riba pia kuna vikundi vingine 5 ambavyo vimenufaika na mikopo hiyo  kupitia fedha za mapato ya ndani kwa robo ya pili.Vikundi hivyo ni  Mama Samia toka Kata ya Bulemeji kimepata mkopo wa shilingi milioni 8,000,000/= Amanina toka toka Kata ya Idedetemya shilingi Milioni 12,000,000/=,Wanawake Songambele toka Kata ya Mondo milioni 10,000,000/= na kikundi cha Mwamko toka Kata ya Idedetemya kimepatia shilingi Milioni 15,000,000/=na kufanya Jumla ya shilingi Milioni 56,365,000/ =ambazo zimekopeshwa mpaka hivi sasa.

Naye, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Misungwi,Bw.Kashinje Machibya amesema Serikali ya awamu ya sita imekuwa ikitekeleza Miradi mbali mbali ya maendeleo na  kuwajali Wananchi wake kwa kuwapatia mikopo ambayo inatolewa na Halmashauri isiyokuwa na riba na bila kubagua Vyama  vya Siasa hapa nchini.

Sambamba na hilo amewataka Kikundi cha Vijana Kazi kufanya kazi kwa bidii na uaminifu ili kurejesha mikopo hiyo kwa wakati na kuruhusu watu wengine kukopa fedha hizo, pia ametaka kuwa na mawazo makubwa ya kukopa fedha zaidi na kuwekeza katika miradi mikubwa yenye tija na maufaa zaidi.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Dkt, Chrispine Shami ameeleza kuwa ni kawaida kila robo ya mwaka wa fedha Halmashauri kutoa mikopo sawa sawa na utaratibu ambao zimewekwa na Serikali na  kutoa wito kwa jamii nzima kupewa elimu juu ya mikopo inayotolewa na Halmashauri isiyokuwa na riba ili waweze kunufaika na mikopo hiyo kwa kufuata masharti,kanuni na taratibu ambazo zimeweka ili waweze kupata mikopo na kurejesha kwa wakati.

Wakati huo huo, Mwenyekiti wa Kikundi cha Vijana kazi cha Kata ya Bulemeji Bw, Dotto Kaji Sylivester ameishukuru Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassani kwa kuwapatia mikopo ya  pikipiki kupitia Halmashauri ambayo itawasaidia kuwanyanyua kiuchumi kwa kupitia pikipiki hizo ambazo wamekabidhiwa hivi mapema wiki hii, na kuahidi kulipa mikopo huo kwa wakati.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Misungwi Bw.Petro Sabato(aliyevaa suti ya kijivu) akimkabidhi kadi ya Pikipiki mwenyeki wa kikundi  cha Vijana Kazi kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Misungwi,ambapo pikipiki hizo zina thamani ya shilingi Milioni 26 mapema wikii hii.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Mhe, Kashinje Machibya,akiwaasa kikundi cha Vijana kazi kuzitumia pikipiki walizopewa kwa manufaa ili kujipatia kipato na kuweza kurejesha mkopo huo kwa wakati ambapo zoezi hilo lilifanyika katika maeneo ya ofisi za Halmashauri siku ya Jumatatu.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Dkt, Chrispine Shami aliyesimama akitoa pongezi kwa kikundi cha Vijana kazi wakati wa makabidhiano ya Pikipiki siku Jumatatu ambapo vijana hao walikabidhiwa pikipiki 10 zenye thamani ya shilingi milioni 26.

 

Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi  Bi.Juliana Mwongerezi akitoa taarifa fupi ya Mradi wa usafirishaji abiria tarehe 30/01/2023 unaotekelezwa na kikundi cha vijana Kazi kata ya Bulemeji,ambapo Kikundi hicho kimekabidhiwa pikipiki 10 zenye thamani ya shilingi milioni 26 ni mkopo kutoka Halmashauri usiokuwa na riba.

Mwenyekiti wa Kikundi cha Vijana Kazi Bw.Dotto Sylivester akitoa shukrani zake za pekee kwa niaba ya vijana wenzake katika ofisi za Halmashauri siku ya Jumatatu,amabapo walipokea pikipiki 10 zenye thamani ya shilingi Milioni 26 kupitia mkopo wa Halmashauri wa bila riba.

Matangazo

  • TANGAZO,KIKAO CHA MADIWANI KWA ROBO YA PILI 2022/2023 February 10, 2023
  • TANGAZO LA MAFUNZO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI -MISUNGWI DC 2022 July 26, 2022
  • TANGAZO USAILI WAKUSANYA MAPATO HALMASHAURI MISUNGWI 2022/2023 August 01, 2022
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI HALMASHAURI YA MISUNGWI June 11, 2022
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • RC Malima atoa Kongole Wananchi Misungwi kujenga Kituo cha Afya kwa Mapato ya ndani

    March 05, 2023
  • DC Misungwi aagiza Miradi ya Maendeleo kukamilika kwa wakati Misungwi

    March 01, 2023
  • Baraza la Madiwani Misungwi lapitisha Bajeti Bilioni 54.6 mwaka wa fedha 2023/2024

    February 22, 2023
  • DC Matiko Paulo Chacha akabidhiwa Ofisi na Mkuu wa Wilaya Iringa Veronika Kessy

    February 08, 2023
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0768867886

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.