• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Baraza la wafanyakazi Misungwi lajadili na kutoa mapendekezo Bajeti ya 2025/2026

Imewekwa : January 21st, 2025

Baraza la Wafanyakazi la Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi lajadili na kupitisha mapendekezo ya Bajeti ya Mapato na Matumizi ya shilingi Bilioni 53.6  kwa mwaka wa fedha 2025/2026 Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Akizungumza wakati wa kikao maalum cha Baraza la Wafanyakazi kwa ajili kutoa mapendekezo ya bajeti  katika ukumbi wa Halmashauri, Mwenyekiti wa kikao ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Misungwi Bw. Addo Missama ameeleza kwamba ni halali kwa kila mfanyakazi kutimiza wajibu wake na kusisitiza ushirikiano ili kuhakikisha wanafikia adhima na malengo yaliyowekwa na kuwaomba Watumishi waendelee kutekeleza majukumu kwa kuzingatia Bajeti iliyopitishwa  .

Bw. Missama ameongeza kuwa kikao hicho ni maalum kwa ajili ya kupitia na kufanya tathmini ya utendaji kazi ambapo kila mfanyakazi ana haki katika utekelezaji wa majukumu na stahiki anapowajibika kutimiza malengo yaliyopangwa hivyo amewasihi kufanya kazi kwa bidii na kwamba hakuna haki bila wajibu na kila mmoja tuendelee kufanya kazi kwa  mujibu wa sharia , taratibu na miongozo.

Awali akiwasilisha rasimu ya Bajeti  ya mwaka 2025/2026 Afisa Mipango wa Halmashauri Bi. Peniel Titus kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi amefafanua kwamba katika rasimu hiyo ya Bajeti kiasi cha shilingi 4,641,245,829/= ni fedha zitokanazo na vyanzo vya Mapato ya ndani ya Halmashauri ,kiasi cha shilingi. Bilioni 41,888,608,000/= ni fedha ya mishahara ya Watumishi, na kiasi cha shilingi Bilioni 1,359,841,000/= ikiwa ni  ruzuku ya uendeshaji ( OC) na kiasi cha shilingi Bilioni 5,725,139,282/= ni kwa ajili ya kutekeleza Miradi ya Maendeleo na fedha zote ni kutoka Serikali kuu.

Bi. Peniel Titus ameeleza kuwa pamoja na kuwepo kwa rasimu ya bajeti hiyo ofisi ya Mipango na Uratibu imeahidi kutekeleza na kufanyia kazi mapendekezo na maadhimio ya kikao hicho ikiwa ni pamoja na kuendeleza ushirikiano ili kuhakikisha kuwa na maendeleo chanya katika jamii ndani ya Halmashauri ya Misungwi.

Kwa upande Mwenyekiti wa TUGHE Mkoa wa Mwanza Bw. Aloysius Mapembe amesema mapendekezo ya  Bajeti hii ya mwaka wa fedha 2025/2026 yamendaliwa na kuwasilishwa kwa weledi na umakini na kupongeza uwasilishwaji wake ambapo pia amempongeza Mwenyekiti wa kikao ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Misungwi kwa kuwa na timu yenye kujituma na kuandaa vyema taarifa ya Bajeti pamoja na kikao hicho.

Baraza hilo la Wafanyakazi limehudhuriwa na wajumbe ambao ni Wawakilishi wa Watumishi wa kila Idara na Vitengo, Wakuu wa Idara  na Vitengo vya Halmashauri ya Misungwi, Viongozi wawakilishi wa Vyama vya Wafanyakazi  kwenye ngazi ya matawi, ngazi ya Wilaya pamoja na Viongozi wa ngazi ya Mkoa.


Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.