• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Baraza la Misungwi Lapitisha Bajeti ya Mapato na Matumizi ya shilingi Bilioni 51.5

Imewekwa : February 2nd, 2024

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi laridhia na kupitisha Bajeti ya Mapato na Matumizi ya shilingi Bilioni 51.5  kwa mwaka wa fedha 2024/2025 Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Akizungumza jana tarehe 1 Februari 2024 wakati wa kikao maalum cha Baraza hilo katika ukumbi wa Halmashauri ,Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Mhe,Kashinje Machibya amesema rasimu hiyo ya Bajeti ya kiasi cha shilingi. Bilioni 51.5 itasaidia kuwaletea wananchi maendeleo ikiwa pamoja na kuongeza na kuboresha miundombinu ya huduma za kijamii kama vile huduma za Sekta ya Elimu, huduma za Afya, maendeleo ya jamii , mazingira, ambapo katika rasimu hiyo kiasi cha shilingi. Bilioni 8.6 zimetengwa kwa ajili ya kutekeleza shughuli za miradi maendeleo.

Mhe, Machibya ameeleza kwamba Baraza la Madiwani halitokuwa tayari kumvumilia Kiongozi ama mfanyabiashara yoyote atakayesababisha na kuleta ukwamishaji katika suala la Ukusanyaji wa Mapato kwa kuzingatia kuwa kipaumbele cha Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ni Mapato, Mapato Mapato kwa mfulululizo kwa lengo kuu la kuwaletea maendeleo Wananchi wa Wilaya hiyo.

Mhe, Machibya amesema kwamba Baraza la Madiwani lina wajibu wa kusimamia mapato ya ndani kwa  bidii  kwa maslahi mapana ya Wananchi na kuhakikisha kutokutoa mwanya wa upotevu wa mapato kwa namna yeyote ile na kuwataka Watendaji wa Kata kuendelea kusimamia  na kutumia kikamilifu fedha za Miradi ya Maendeleo katika Kata zao  vizuri na  ziendane thamani ya fedha katika miradi hiyo wanayoisimamia.

Awali akiwasilisha rasimu ya Bajeti  ya mwaka 2024/2025 Afisa Mipango Bi. Peniel Titus kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi amefafanua kwamba katiaka rasimu hiyo ya Bajeti kiasi cha Bilioni 4.7 ni fedha zitokanazo na vyanzo vya Mapato ya ndani ya Halmashauri ,kiasi cha shilingi. Bilioni 36.7 ni fedha ya mishahara ya Watumishi,kiasi cha shilingi Bilioni 1.3 ni  ruzuku ya uendeshaji ( OC) na kiasi cha Bilioni 8.6 ni kwa ajili ya kutekeleza Miradi ya Maendeleo na fedha zote ni kutoka Serikali kuu.

Kwa upande wake Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Misungwi  Bw. Leonidas Kondela ameipongeza Halmashauri kwa kubuni na kupanga kuanzisha ujenzi wa Shule ya awali na Msingi itakayowezesha watoto wa Wilaya ya Misungwi kupata elimu bora na ya uhakika pia amewaomba kwa msisitizo Waheshimiwa Madiwani, Wakuu wa Taasisi mbalimbali za Serikali  na Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja na Wataalam wote kuhakikisha wanasimamia fedha za Miradi ya maendeleo kwa umakini mkubwa ili kuwaletea maendeleo wananchi.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri Bw.Joseph Mafuru amesema Bajeti hii ya mwaka wa fedha 2024/2025 ni lazima itekelezwe kwa kuchukua hatua madhubuti katika ukusanyaji wa mapato ya ndani pamoja na fedha zinazotoka Serikali kuu kwa ajili Miradi mbalimbali ya maendeleo zitasimamiwa vizuri kwa maslahi mapana ya Wananchi ambapo shilingi. Milioni 300 kutoka mapato ya ndani zitaweza kutekeleza ujenzi wa shule ya awali na msingi na kuwanufaisha watoto wa Wilaya ya Misungwi na kuwa chanzo kimojawapo cha mapato ya ndani yenye uhakika.

Wakati huo huo,Diwani wa Viti Maalum Dotto Sembelu  amesema Bajeti ya kiasi cha shilingi. Bilioni 51.5 ambapo kati hizo kiasi cha shilingi  Bilioni 4.7 ni fedha za mapato ya ndani ya Halmashauri, ameeleza kuwa  Madiwani na Watendaji wanawajibu wa kusimamia ukusanyaji wa mapato  pamoja na kuhakikisha fedha hizo zinapatikana na kwenda kufanya shughuli za maendeleo  kwa wananchi pia amemshukuru  Mhe, Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi za miradi ya maendeleo ikiwemo fedha za ujenzi wa madarasa na ujenzi wa shule mpya ya Sekondari wa ajili utekeleza wa Miradi mbalimbali ya maendeleo.

Waheshimiwa Madiwani wakijadili na kupitisha Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa  Mwaka 2024/2025 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi tarehe 01/20/2024.

Wakuu wa Taasisi,Idara na Vitengo wakisikiliza na kujadili Bajeti ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2024/2025 mapema jana katika ukumbi wa Halmashauri ambapo Bazara limepitisha Bajeti ya shilingi Bilioni 51.5

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.