• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Baraza la Madiwani Misungwi lapongeza Walimu,Shirika la ASAP latoa motisha ya Fedha

Imewekwa : November 14th, 2022

Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi yatoa Tuzo na Zawadi kwa Walimu mahiri 49 wa Shule za msingi na Sekondari waliofanya vizuri katika Shindano lililoandaliwa kwa lengo la kutoa motisha kwa Walimu Mkoani Mwanza.

Akizungumza katika Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Misungwi, lililofanyika katika ukumbi wa Halmashauri mgeni rasmi ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe, Veronika Kessy amesema kwamba kuna umuhimu kwa Walimu kupata motisho kutokana na utendaji kazi mzuri  wenye kuleta tija katika Sekta ya Elimu.

Bi, Veronika Kessy ametoa pongezi za dhati kwa Shirika hilo lisilo la Kiserikali kwa kujitokeza katika kufadhali baadhi ya Shule za Msingi na Sekondari katika Kata za Idetemya na Mwaniko kwa kutoa misaada mbalimbali ikiwemo kukarabati vyumba vya madarasa,matundu ya vyoo na kujenga vyumba vya madarasa katika shule hizo.

Kwa upande wake Mratibu wa Shirika lisilokuwa la kiserikali la Africa School Assistance Project Bw, Jackson Mzenya ameeleza kuwa shirika hilo linafanya kazi katika Mikoa miwili Arusha na Mwanza,ambapo kwa Mwanza wamejikita katika Wilaya ya Misungwi pamoja na jamii zake na kufanikiwa kufanya kazi katika shule 8 kuanzia 2014 hadi 2022,ambapo lengo la shirika ni kutanua wigo wa kutoa huduma kusimamia na kuboresha shule ambazo ziko nje ya miji zinapata Elimu bora na wanafunzi kutimiza ndoto zao.

Bw, Mzemya alifafanua kuwa Tuzo hizo za Walimu zimetolewa baada ya kufanya shindano lililoshirikisha Shirika la Africa School Assistance Project pamoja na Shirika la The Foundation For Tomorrow ambapo wameweza kupata Walimu 49 miongoni mwao Walimu 35 kutoka Shule za msingi na Sekondari wamepata Zawadi ya vyeti na fedha shilingi 500,000/= kila mmoja kwa jumla ya shilingi 17,500,000/= na Walimu 14 wamepatiwa vyeti pekee ikiwa ni motisha na kuwaongezea chachu katika uwajibikaji katika kufundisha Wanafunzi.

Wakati huo huo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Mhe, Kashinje Machibya kwa niaba ya Barazala Madiwani la Halmashauri  amesema na kuwasihi Walimu wote kuendelea na moyo na kutekeleza majukumu yao kwa ufasaha na kuwa waadilifu na wasithubutu kuchezea fedha za umma ambazo zinatolewa na Serikali kutekeleza miradi  mbalimbali katika sekta ya elimu. 

Naye Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Misungwi Bw. Benson Mihayo ameshukuru Shirika hilo kwa kuendelea kufadhili baadhi ya shule za Elimu ya Msingi na Sekondari na kuwaomba waende mbali zaidi katika shule ambazo ziko pembezoni mwa Wilaya ya Misungwi kutoa huduma bora ambapo itapelekea chachu ya maendeleo ya Elimu katika Shule hizo.

Bw. Benson Mihayo amesisitiza kupitia shirika hilo wamejipanga kimkakati kuhakikisha wanashirikiana bega kwa bega kuinua Elimu katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa kuwapongeza Walimu kwa kutoa zawadi na vyeti kwa wale ambao wafanya vizuri zaidi kwa lengo la kwa motisha kuendelea kutoa huduma iliyo bora katika vituo vyao vya kazi.

Mmoja wa Walimu waliopata Zawadi ya Cheti na Fedha taslimu shilingi 500,000/= Bw, Leonald Maige kutoka shule ya msingi Misungwi, amesema kwamba amepata faraja na Amani baada ya kupata Zawadi ya Cheti na fedha shilingi 500,000/= na kueleza kuwa Walimu ni wito na kujituma kwa bidii ambapo amewashauri Walimu wengine kipindi kijacho watumie fursa hii n akushiriki katika shindano la kupata Walimu mahiri na bora kwa lengo la kupata motisha na kuongeza ari na moyo wa kufanya kazi ya kufundisha kwa manufaa ya Halmashauri na taifa kwa ujumla.

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi katikati Mhe,Veronika Kessy akiwa na viongozi mbalimbali waliohudhuria katika hafla fupi ya kuwapongeza walimu mahiri katika ukumbi wa halmashauri ya Wilaya ya Misungwi siku ya Ijumaa.




Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.