• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Baraza la Madiwani Misungwi lapitisha Bajeti Bilioni 54.6 mwaka wa fedha 2023/2024

Imewekwa : February 22nd, 2023

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Misungwi lapitisha rasmi ya Bajeti ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2023/2024 yenye jumla ya shilingi Bilioni 54.6 Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Akizungumza jana mapema wakati wa kikao maalum cha Baraza hilo katika ukumbi wa Halmashauri ,Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Mhe,Kashinje Machibya amesema rasimu hiyo ya Bajeti ya kiasi cha Bilioni 54.6 , Bilioni 4.8 ni fedha zitokanazo na vyanzo vya Mapato ya ndani ya Halmashauri ,kiasi cha Bilioni 40.6 ni ruzuku ya mishahara,kiasi cha Bilioni 1.02 ni  ruzuku ya uendeshaji, itasaidia kuwaletea wananchi maendeleo ikiwa pamoja na kuongeza na kuboresha miundombinu ya huduma za kijamii kama vile umeme maji na huduma za Afya,ambapo katika rasimu hiyo kiasi cha Bilioni 7.7 kimetengwa kwa ajili ya fedha za miradi maendeleo.

Mhe, Machibya amesema kwamba Baraza la Madiwani lina wajibu wa kusimamia mapato kwa bidii  kwa maslahi mapana ya wananchi na kuhakikisha kutokutoa mwanya wa upotevu wa mapato kwa namna yeyote ile na kuwataka watendaji wa Kata kuendelea kusimamia  na kutumia kikamilifu fedha za Miradi ya Maendeleo katika Kata zao  vizuri na  ziendane thamani ya fedha katika miradi hiyo wanayoisimamia.

Awali akiwasilisha rasimu hiyo kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bi.Mwanajumbe Zuberi ambaye ni Afisa Mipango ameeleza katika rasimu hiyo ya Bajeti kiasi cha Bilioni 54.6, Bilioni 4.8 ni fedha zitokanazo na vyanzo vya Mapato ya ndani ya Halmashauri ,kiasi cha Bilioni 40.6 ni ruzuku ya mishahara,kiasi cha Bilioni 1.02 ni  ruzuku ya uendeshaji ( OC) na kiasi cha Bilioni 7.7 ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo na fedha hizo ni kutoka Serikali kuu.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Wilaya ya Misungwi Bw.Petro Sabato  kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, amesisitiza kwa Waheshimiwa Madiwani, Taasisi mbalimbali za Serikali na Viongozi na Wataalam wote kuhakikisha wanasimamia fedha za Miradi ya maendeleo kwa umakini mkubwa ili kuwaletea maendeleo wananchi.

Naye Kaimu Mkurugenzi Bw.Benson Mihayo amesema rasimu ya Bajeti ya mwaka wa fedha 2023/2024 ni lazima itekelezwe kwa kuchukua hatua madhubuti katika ukusanyaji wa mapato ya ndani lakini pamoja na fedha zinazotoka Serikali kuu kwa ajili Miradi mbalimbali ya maendeleo zisimamiwe vizuri kwa maslahi mapana ya Wananchi.

Diwani wa Kata Mbarika  na Mwenyekiti wa Kamati Huduma za Jamii Mhe,Joel Dogani amesema Bajeti ya kiasi cha Bilioni 54.6 ambapo kati hizo kiasi cha Bilioni 4.8 ni mapato ya ndani ya Halmashauri, ameeleza kuwa wanawajibu wa kusimamia ukusanyaji wa mapato  pamoja na kuhakikisha fedha hizo zinapatikana na kwenda kufanya shughuli za maendeleo  kwa wananchi pia amemshukuru  Mhe, Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi za miradi ya maendeleo ikiwemo fedha za UVIKO kwa ajili utekeleza wa Miradi mbalimbali ya maendeleo.

Baadhi ya Viongozi mbalimbali na Washeshimiwa Madiwani wakiendelea kujadili na kupitisha Bajeti yenye jumla ya kiasi cha Bilioni 54.6 ya mwaka kwa fedha 2023/2024 katika ukumbi wa Halmashauri hapo jana.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya misungwi Mhe,Kashinje Machibya aliyesimama akiongoza mkutano wa Baraza wakati wa kupitisha bajeti yenye kiasi cha Bilioni 54.6 ya mwaka kwa fedha 2023/2024 katika Ukumbi wa Halmashauri siku ya Jumanne tarehe 21/02/2023

Matangazo

  • TANGAZO,KIKAO CHA MADIWANI KWA ROBO YA PILI 2022/2023 February 10, 2023
  • TANGAZO LA MAFUNZO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI -MISUNGWI DC 2022 July 26, 2022
  • TANGAZO USAILI WAKUSANYA MAPATO HALMASHAURI MISUNGWI 2022/2023 August 01, 2022
  • TANGAZO LA MAOMBI YA MIKOPO YA VIKUNDI HALMASHAURI YA MISUNGWI June 11, 2022
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • RC Malima atoa Kongole Wananchi Misungwi kujenga Kituo cha Afya kwa Mapato ya ndani

    March 05, 2023
  • DC Misungwi aagiza Miradi ya Maendeleo kukamilika kwa wakati Misungwi

    March 01, 2023
  • Baraza la Madiwani Misungwi lapitisha Bajeti Bilioni 54.6 mwaka wa fedha 2023/2024

    February 22, 2023
  • DC Matiko Paulo Chacha akabidhiwa Ofisi na Mkuu wa Wilaya Iringa Veronika Kessy

    February 08, 2023
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0768867886

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.