• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Baraza la Madiwani laridhia na kupitisha Makisio ya Bajeti ya Mapato na Matumizi ya Billioni 56.5 kwa mwaka 2019/2020 Misungwi.

Imewekwa : January 19th, 2019

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi,Mkoani Mwanza limepitisha Makisio ya Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2019/2020 ya kukusanya na kutumia shillingi Billioni 56.5  kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya maendeleo, Mishahara ya Watumishi pamoja na matumizi ya kawaida .

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Mhe Antony Bahebe Masele alieleza haya katika Mkutano wa Baraza maalum la Madiwani lililofanyika katika Ukumbi wa MGS Mjini Misungwi hivi karibuni, kwa ajili  ya kujadili na kupitisha makisio ya Bajeti ya mapato na matumizi ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha wa 2019/2020 ambapo Halmashauri imeweka makisio ya kukusanya kiasi cha fedha Billioni 56,5 zitokanazo na Mapato ya Ndani ya Halmashauri, na ruzuku toka Serikalini.

Akiwasilisha  taarifa ya Makisio ya Bajeti hiyo , Afisa Mipango wa Halmashauri , Bi Anna Urioh kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri  alisema kwamba katika mwaka wa fedha  2019/2020 Halmashauri ya Misungwi imepanga kukusanya na kutumia Bajeti ya fedha yenye jumla ya shillingi Billioni 56,516,376,608/= ambapo kati ya fedha hizo, shilingi 2,830,722,000/= zitatokana na Mapato ya ndani ya Halmashauri , shillingi 37,830,717,000/= ni fedha kwa ajili ya Mishahara ya Watumishi ,shillingi  14,838,549,323/= ni bajeti ya fedha kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi ya Maendeleo pamoja na shillingi 1,047,110,285 /= ni fedha za ruzuku ya Serikali kwa ajili ya matumizi ya kawaida .


Afisa Mipango wa Halmashauri Bi, Anna Urioh akiwasilisha Makisio ya Bajeti ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2019/2020 katika Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupitisha na kubariki 

Bi,Anna Urioh alifafanua kwamba Halmashauri ya  Wilaya ya Misungwi katika Bajeti ya mapato ya ndani kwa mwaka 2019/2020 ya shillingi 2,830,722,000/= imekuwa na ongezeko la makadirio ya kukusanya Mapato ya shilling 421,951,000/= ukilinganisha na makisio ya  Bajeti ya mapato ya ndani ya mwaka 2018/2019 ambayo yalikuwa ni shillingi 2,408,771,000/= ambapo hadi kufikia mwezi Disemba 2018 Halmashauri ilikuwa imekusanya jumla ya shillingi 824,133,778/= sawa na asilimia 34%  ya makusanyo ya Mapato yote.

Mkurugenzi Mtendaji Wilaya Bw, Kisena Mabuba akizungumza jambo katika majadiliano ya Makisio ya Bajeti ya mwaka 2019/2020 katika Mkutano wa Baraza la Madiwani.

Afisa Mipango huyo aliongeza kwamba ongezeko la bajeti ya mapato ya ndani katika Bajeti ya  mwaka 2019/2020 limetokana na  kuzingatia mapendekezo ya Kamati mbalimbali za Halmashauri pamoja na Menejimenti kubuni  vyanzo vipya na kuwa na takwimu nzuri na halisi ya Wafanyabiashara wa aina mbalimbali ikiwemo Machinjio, Minada , Standi, Madini, na mengine .

Mhe, Antony Bahebe Masele alisema kuwa Baraza la Madiwani la Halmashauri hiyo limejipanga kikamilifu katika kusimamia na kufuatilia kwa makini utekelezaji wa Bajeti iliyopitishwa, hususani katika suala la ukusanyaji wa Mapato ya ndani ambayo yameongezeka katika bajeti ya mwaka ujao na Madiwani watahakikisha wanashirikiana kwa dhati na Watendaji wote ili kuweza kufika malengo ya kukusanya mapato hayo na kueleza kuwa vyanzo vipo vingi cha muhimu ni uwajibikaji na usimamizi mzuri.

Alisisitiza na kueleza kwamba Baraza la Halmashauri hiyo litawachukulia hatua za Kinidhamu Watendaji wote watakaoshindwa ama kuzembea katika jukumu la ukusanyaji wa Mapato na Madiwani watahakikisha wanafuatilia chanzo kimoja kimoja na kuwaomba Watendaji kuwajibika ipasavyo na kuhakikisha vyanzo vyote vinakusanywa kwa asilimia zote na kufikia malengo.

Baadhi ya Madiwani wakifuatilia mjadala na maoni ya Makisio ya Bajeti katika Mkutano wa Baraza la Madiwani la Bajeti

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo,Bw,Kisena Mabuba alisema kwamba Menejimenti ya Halmashauri katika maandalizi ya bajeti ya mwaka 2019/2020 imezingatia maelekezo mbalimbali ya Serikali ya wamu ya tano ya kisekta pamoja na  malengo ya Wilaya na Vipaumbele vya kiwilaya ambavyo vinalenga kujibu matarajio ya Serikali ya awamu ya tano, na kulingana na Mwongozo wa bajeti uliotolewa.

Bw, Kisena Mabuba amewataka Madiwani pamoja na Watendaji wa Halmashauri kuhakikisha wanatekeleza shughuli zaa Halmashauri pamoja na miradi ya Maendeleo kwa kuzingatia na kufuata Bajeti kama ilivyopitishwa na kuidhinishwa na Serikali na kuhakikisha Ukusanyaji wa Mapato ya ndani unafikia malengo kupitia vyanzo vyote vilivyoanishwa.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.