• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Baraza la Madiwani lapitisha rasimu ya Bajeti ya shilingi Bilioni 44.3 mwaka 2021/2022 Misungwi.

Imewekwa : February 17th, 2021

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Mkoani Mwanza laridhia na kupitisha rasimu ya Bajeti ya mapato na matumizi ya shilingi Bilioni 44.3 kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Akizungumza katika Mkutano  maalum wa Baraza hilo Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Kashinje Erasto Machibya amesema kwamba Halmashauri ya Misungwi imepanga kukusanya na kutumia jumla shilingi Bilioni 44.3 katika mwaka  wa fedha 2021/2022 ambapo fedha hizo ni kutokana na vyanzo vya mapato ya ndani ya Halmashauri yenye jumla ya shilingi Bilioni 2. 4 pamoja na fedha za ruzuku toka Serikali kuu  shilingi  Biliioni 41.8.

Mhe, Kashinje amesema katika Bajeti hiyo Baraza limeridhia mpango wa ujenzi wa Kituo cha Afya kwa gharama ya shilingi milioni 400 fedha ambayo inatokana na mapato ya ndani ya Halmashauri pamoja na kuendelea  kukamilisha miradi mingine katika sekta ya Afya, Elimu, Maji, Umeme, Mazingira na mingineyo.

Amewataka Madiwani kuwa na utamaduni wa kusimamia miradi ya maendeleo vizuri inayotekelezwa katika maeneo yao na kwamba wanapaswa kufahamu fedha zote zinazotolewa na Serikali pamoja na michango ya wadau na nguvu ya Wananchi yote isimamiwe kikamilifu na miradi itekelezwe kwa kiwango na ubora.

Akiwasilisha rasimu hiyo ya Bajeti ya Halmashauri kwa mwaka 2021/2022, kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Kaimu Afisa Mipango Mwanajumbe Zuberi amesema katika mwaka wa Fedha 2021/2022 Halmashauri imetenga jumla ya shilingi Bilioni 44,324,862,080. na kati ya hizo shilingi  Bilioni  2,498,951,580. zitatokana na Mapato ya Ndani (Own source) na shilingi Bilioni 41,825,910,500. ni fedha kutoka serikali kuu  na kati ya fedha yote inayotoka serikali kuu shilingi, Bilioni 35,498,052,000. ni kwa ajili ya kulipa mishahara ya watumishi wa Halmashauri, ambayo ni sawa na asilimia 84.87 ya Bajeti yote inayotoka Serikalini.

Alieleza kwamba katika bajeti hiyo  jumla ya shilingi Bilioni  1,443,559,000. ni Ruzuku kutoka Serikali kuu kwa ajili ya matumizi ya kawaida (OC), shilingi Bilioni  4,884,299,500. ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo, na shilingi Bilioni 35,498,052,000. ni kwa ajili ya Mishahara ya Watumishi pia Halmashauri imetenga jumla ya shilingi Milioni. 713,608,632. kutoka katika Mapato ya Ndani kwa ajili ya kutekeleza shughuli za Maendeleo. 

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, Kisena Mabuba amesema makisio ya Bajeti hiyo yamelenga kuwaletea maendeleo Wananchi wa Wilaya ya Misungwi kutokana na kubuni vyanzo vya mapato vipya  ikiwa ni pamoja na kutenga fedha za fidia ya ardhi  kwa ajili ya kutwaa maeneo kikiwemo Kisiwa cha Buzumo Kata ya Mbarika ambacho matarajio ya kuwekeza kuwa eneo la utalii kwa kuweka Wanyama wasio wakali na kuimarisha utalii na kuwa chanzo cha mapato ya Halmashauri.

Bw, Kisena Mabuba ameeleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi imeweka mipango na mikakati ya kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa viwango na suala la ukusanyaji wa mapato ya ndani unafanyika kwa uadilifu na uaminifu na fedha yote inaelekezwa katika maeneo yaliyopangwa na kukusudiwa na hakutokuwepo kwa ubadhilifu wowote.

Kwa upande wake Katibu Tawala Wilaya ya Misungwi, Petro Sabatto ambaye alimwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Juma Sweda amesema kwamba amepongeza juhudi zilizofanywa na Wataalam na kundaa Bajeti nzuri na kuwataka Madiwani kusimamia kikamilifu miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao na kuhakikisha inakuwa ya viwango na thamani ya fedha inaonekana.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.