• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Balozi wa Pamba nchini Mhe,Aggrey Mwanri Atoa Mbinu Bora Kilimo cha zao la Pamba Wilayani Misungwi

Imewekwa : October 11th, 2023


Balozi wa Pamba nchini Mhe,Aggrey Mwanri aagiza Watendaji na Wataalamu kutoa Elimu kwa Wakulima kuhusu  kilimo  cha kisasa cha zao la Pamba Wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.

Agizo limetolewa  na Mhe,Aggrey Mwanri katika ziara ya kutembelea na kuelimisha Wananchi kwa siku nne katika Vijiji 11 katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi ambapo aliwataka Wataalamu wa Kilimo kuendelea kuelimisha Wakulima katika maeneo yao kwa kulima zao la pamba kitaalamu na kwa tija  ili kuzalisha mazao mengi katika eneo dogo.

Mhe, Mwanri ametoa wito huo kwa Maafisa Kilimo na Watendaji wa Kata kuendelea kutoa mafunzo kwa Wananchi juu ya kilimo cha  kisasa cha zao la pamba kwa kutumia mbegu bora na namna sahihi ya matumizi ya viuatilifu na  kufuata maelekezo ya wataalamu watakayopatiwa katika mafunzo  ili kuongeza pato kwa ngazi ya kaya na Halmashauri kwa ujumla.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Misungwi Mhe, Abdi Makange kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe,Paulo Chacha amesistiza nidhamu kwa watumishi wa umma  kuwa na nidhamu ya kazi ili kuwatumikia Wananchi kikamilifu  kuheshimiana na kushirikiana kwa pamoja na hatosita kumchukulia hatua mtumishi yoyote atakaye kwenda kinyume na maagizo alioyatoa ,pia ameagiza kila mwananchi alime heka moja ya zao la pamba ili kufikia malengo yalio kusudiwa.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bw.Christopher Legonda ameelekeza kwa watendaji wote ngazi ya kata na vijiji kuhakikisha wanahamasisha wananchi kujiandaa na kilimo katika maeneo yao ili kuendana na msimu wa mvua kwa kufuata ushauri wa wataalamu wa kilimo.

Kwa upande mwingine Bw.Legonda amesema kuwa zoezi la  dirisha la uandikishaji kwa watoto wanaotakiwa kujiunga na elimu ya Awali na darasa la kwanza lifanyike mapema kabla ya tarehe 30 Disemba Mwaka huu na maandalizi  ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza .

Naye Afisa Kilimo wa Wilaya ya Misungwi Bi, Esther Mcharo amesema kuwa wakulima wanatakiwa kufuata ushauri  wa wataalamu  namna ya kulima kisasa zao la pamba ili kuleta tija na kupata mazao mengi ambapo amewataka wakulima kufuata kanuni kumi za namna ya kulima zao la pamba ikiwa ni pamoja na kutayarisha shamba mapema kutumia mbolea za samadi ,kupanda pamba mapema,kupanda kwa mstari na kwa idadi halisi ya mbegu katika kila shimo na kupalilia kwa wakati ili kuvuna pamba na kuichambua mapema huku unyunyuziaji wa dawa ukizingatiwa wakati wa ulimaji huo.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Kanyelele Bw,Thomas Ishunasho ametoa shukrani za pekee kwa ujio wa Balozi wa pamba hapa nchini kwa kutoa mafunzo ya kilimo cha kisasa cha zao la pamba kwa Wilaya ya Misungwi ambapo kwa kupitia mafunzo hayo wameweza kupata elimu ya kutosha na kuahidi kwenda kuwaelimisha wananchi namna nzuri ya kulima zao la pamba katika kata zao.

Balozi wa Pamba nchini Bw,Aggrey Mwanri akielekeza na namna ya unyunyuziaji wa dawa katika zao la pamba wa kufuata mistari ya halisi ya eneo la shamba.

Wataalamu wa Kilimo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi wakionyesha namna ya uchimbaji wa mashimo wakati kupamba mbegu bora za zao la pamba.



Mkuu wa Idara ya Kilimo,Ufagaji na Uvuvi Dr Crispine Shami akisoma taarifa fupi  ya ziara katika Ukumbi wa Halmashauri leo mapema ambapo alitoa shukrani kwa kufanyika Mafunzo ya namna ya kulima kisasa zao la pamba katilka Wilaya ya Misungwi.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.