• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Waziri Mwigulu awahakikishia kukamilika kwa miradi ya maji Usagara awataka Wananchi Misungwi kuunga juhudi za Rais Samia.

Imewekwa : September 16th, 2024

Waziri wa Fedha Mhe, Mwingulu Nchemba awahakikishia Wananchi wa Wilaya ya Misungwi kuwa Serikali itaendelea kukamilisha utekelezaji wa Miradi ya maji ya Ukiriguru na mingine ambayo imesuasua kutokana na changamoto za fedha na Wizara imeshachukua hatua za malipo ya miradi  husika Wilayani Misungwi.

Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba ameyabainisha hayo  tarehe 15 Septemba, wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya Taasisi ya  Chuo cha Uhasibu Tanzania Kampasi ya Mwanza (TIA), iliyojengwa na Serikali kwa gharama ya shilingi Bilioni 7.8, kitakachokuwa na uwezo wa kuhudumia wanafunzi zaidi ya 5,000 kwa wakati mmoja, na kuahidi kuwa Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan, imewekeza rasilimali fedha katika sekta mbalimbali za maendeleo ikiwemo sekta ya elimu pamoja sekta ya maji na miumdombinu ya barabara na kuwataka Wananchi kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais Samia ambapo Wizara ya fedha tayari imeshaandaa malipo ya Mkandarasi  wa mradi wa Maji wa Ukirigurtru hadi Usagara na  Serikali itaendelea kutoa fedha kwa awamu ili kukamilisha miradi hiyo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Alexander Mnyeti, amezungumzia changamoto zinazokabili miradi ya maji katika jimbo la Misungwi amesema kuwa Mkandarasi anasuasua sana wa mradi wa Maji wa vijiji 16 kutoka chanzo cha maji cha Ihelele ameomba Wizara itatue na kuweka Mkandarasi mwingine ili utekelezaji ukamilike kwa haraka pamoja na kusuasua kwa mradi wa maji wa Ukiriguru hadi Usagara unaotekelezwa polepole sana kwa sababu Mkandarasi hajalipwa fedha kitendo ambacho kinasababisha kusuasua kwa mradi huo na kumsisitiza Waziri Nchemba aweze kushughulikia na kuhakikisha Wakandarasi wanalipwa kwa wakati na miradi ikamilike na hatimaye kukidhi matarajio ya Wananchi wa Misungwi.

Mhe. Mnyeti ameongeza kwamba sambamba na miradi ya maji  pia ameomba kulipwa kwa Mkandarasi wa barabara ya Mwanangwa – Misasi hadi Kahama ambaye amesimama kutokana na madai ya fedha ili kuendelea na kazi katika barabara hiyo muhimu kwa uchumi na huduma za kijamii pamoja na kuongeza Vifaa tiba vya thamani ya shilingi milioni 500 katika Hospitali ya Wilaya ya Misungwi ili Wananchi wapate huduma bora ya kisasa.

Mhe, Nchemba ameipokea changamoto ya Miradi ya maji kuhusu kususua kwa  Wakandarasi na kuweka wazi kwamba Wizara ya fedha itahakikisha inakamilisha  malipo na hundi ipo tayari kwa ajili ya kumlipa Mkandarasi huyo wa mradi wa Maji wa Ukiriguru hadi Usagara ambaye hajalipwa malipo hayo ambayo yataongeza kasi ya utekelezaji wa mradi huo wa maji ambao umelenga kuwakomboa na kuboresha maisha ya Wananchi wa Usagara na Wilaya ya Misungwi.

Akitoa salamu za Wilaya kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe. Johari Samizi, ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita, inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kuipatia Wilaya yake, zaidi ya shilingi Bilioni 39 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika Wilaya hiyo katika kipindi cha miaka mitatu ambazo zimeelekezwa kutekeleza miradi mbalimbali ikiwemo sekta za afya, elimu na maji.




Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.