• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Benjamin Mkapa Foundation watoa msaada wa Vifaa wezeshi vya uzazi salama kwa Wajawazito na Watoto kwenye Vituo vya Afya Misungwi

Imewekwa : August 17th, 2019

Taasisi ya Benjamin Mkapa Foundation yatoa misaada ya Kompyuta tano na Vifaa wezeshi 6 vya kujifunzia uzazi salama  katika Vituo vitano vya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa lengo la kupunguza Vifo vitokanavyo na uzazi kwa  akina Mama Wajawazito na watoto chini ya umri wa miaka mitano.

Akizungumza katika makabidhiano ya msaada wa vifaa hivyo katika Hospitali ya Wilaya ya Misungwi, Afisa Mradi Vijijini Kanda ya Ziwa  wa Taasisi ya Benjamin Mkapa, Bi,  Scholastica Komba amesema kwamba msaada huo ni pamoja na Kompyuta tano aina ya Dell, Midoli ya Mwanasesele 6 kwa ajili ya kujifunza namna ya uzazi salama kwa akina mama na Baby Natalia 6 ambavyo vifaa hivyo vitasaidia vituo vya Afya hivyo  kutoa mafunzo kwa Wauguzi namna ya kumsaidia mtoto aliyezaliwa na shida ya kupumua ambavyo vyote vinathamani ya shilingi Milioni 60.

Bi, Scholastica Komba Afisa Mradi Vijijini Kanda ya Ziwa wa Tasasisi ya Benjamin Mkapa Foundation akimkabidhi Vifaa wezeshi Baby Natalia vya kujifunzia Wauguzi namna ya uzazi salama kwa Wajjawazito na watoto wachanga,kwa lengo la kupunguza Vifo vitokanavyo na uzazi kwa Wajawazito kwa Mganga Mkuu wa Wilaya Dkt, Zabron Masatu,katika Hospitali ya Wilaya ya Misungwi.

Bi, Scholastica Komba alieleza kuwa lengo ni kusaidia Vituo vya kutolea huduma  za Afya kuona matokeo chanya kwa akina mama Wajawazito wakati wa kujifungua pamoja na  watoto wanapozaliwa, na vifaa hivyo vitawasidia Wauguzi na Wakunga kupata ujuzi zaidi na uzoefu wa kuwahudumia akina mama Wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua salama na kuhakikisha kwamba Vifo vitonavyo na uzazi kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga vinapungua.

Naye Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya  Misungwi, Dkt, Zabron Masatu alisema kuwa katika Halmashauri ya Misungwi kuna upungufu wa Vitendea kazi ikiwemo na Kompyuta kwa Wataalam wa Sekta ya  Afya, hivyo vifaa hivyo vitasaidia sana katika utendaji kazi na kuongeza ufanisi pamoja na kuleta tija  katika utoaji wa huduma za matibabu kwa Wagonjwa na hatimaye kupunguza Vifo vya akina mama Wajawazito na watoto wachanga .

 Alisema Vifaa hivyo vitapelekwa katika Zahanati ya Mahando, Nyamijundu, Mwaniko, Mwamboku pamoja na Kituo cha Afya Mbarika kwa lengo la kuboresha na kuimarisha utoaji wa huduma za Afya katika maeneo husika.

Bi, Scholastica Komba, Afisa Mradi Vijijini Kanda ya Ziwa, wa Taasisi ya Benjamin William Mkapa Foundation (kulia) akimkabidhi Kompyuta moja kati ya tano zilizotolewa msaada kwa Mganga Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Dkt, Zabron Masatu kwa ajili ya kuwezesha na kuboresha huduma za Afya katika Vituo vitano vya kutolea huduma katika Halmashauri ya Wilaya hii.(kushoto) ni Rose Baluhya Muuguzi katika Hospitali ya Wilaya ya Misungwi akishuhudia makabidhiano hayo hivi karibuni.

Dkt, Zabron  Masatu ameishukuru sana taasisi ya Benjamin Mkapa Foundation kwa kutoa msaada huo katika kipindi hiki cha mahitaji makubwa ya vifaa vya kuwezesha huduma za Afya kuwa bora na kuunga juhudi za Serikali ya awamu ya tano katika kuboresha huduma za Afya hapa nchini.

Mganga Mkuu huyo ameeleza kwamba Vifaa hivyo zikiwemo Kompyuta watahakikisha vinatumika katika uwekaji na utunzaji wa takwimu na kumbukumbu za Wagonjwa na shughuli zote za kitabibu kwenye Vituo hivyo vya kutolea huduma za Afya sambamba na Vifaa vya kujifunza namna ya uzazi salama pamoja na matumizi ya Vifaa vya kujifunzia Wauguzi na Wakunga  namna ya  kumsaidia kupumua mtoto aliyezaliwa na shida ya kupumua na watahakikisha kwamba vifaa vyote vitatunzwa vizuri na kudumu kwa muda mrefu.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.