• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Rais Magufuli awataka Wananchi Misungwi kuchangamkia ajira ujenzi wa Daraja Kigongo - Busisi

Imewekwa : December 7th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Dkt. John Pombe Magufuli amewataka Wananchi wa Wilaya ya Misungwi hususan  vijana wa maeneo ya karibu na mradi wa ujenzi wa daraja la Kigongo –Busisi kuchangamkia fursa za ajira ili kuongeza kipato na hatimaye kupata maendeleo.

Rais Magufuli amesema hayo leo wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la msingi la ujenzi wa Daraja la Kigongo – Busisi ambalo litakuwa na urefu wa kilomita 3.2 kwenye Ziwa Victoria,  linalounganisha Wilaya ya Sengerema na Misungwi, Mkoani Mwanza.

“Natoa wito kwa Wananchi wa karibu wapewe kipaumbele ili watumie fursa hii kupata ajira, wakiwemo vijana na mama lishe ili waweze kuongeza kipato na kujiletea maendeleo yao binafsi na familia zao,”alisema Rais Magufuli, pia amemtaka Mkandarasi huyo kuhakikisha mradi huu unakamilika kwa wakati hivyo wafanye kazi usiku na mchana,

Rais Dkt, John Pombe Magufuli akikata utepe katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa daraja la Kigongo- Busisi Wilayni Misungwi.(wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Tanzania, Kamanda,Simon Sirro, na wa pili kushoto ni Mkuu wa Majeshi ya ulinzi nchini Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo pamoja na Mama Janety Magufuli Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (kulia)

Baadhi ya Wananchi wakiwemo Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Misungwi waliofurika kwa ajili ya kushuhudia uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa Daraja la Kigongo - Busisi (wa kwanza kulia ni Mwamba Makune Diwani wa Kata ya Misungwi)

Rais Magufuli amesema mradi huu unatekelezwa kwa fedha za ndani ya nchi na kubainisha baadhi ya manufaa ya mradi ni pamoja na kujenga uchumi na kukuza biashara za nchi mbalimbali za Rwanda, Burundi na Congo, kuondoa kero ya usafiri  kwa kutumia masaa zaidi ya mawili na nusu kwa Kivuko kwa sasa,  ambapo kwa kutumia Daraja itakuwa unatumia  dakika 4 tu, na kurahisisha usafirishaji wa abiria na mizigo kwa haraka.

Rais Dkt, John Pombe Magufuli amesema Serikali imetenga fedha shilingi Bilioni  3.45 kwa ajili kulipa fidia kwa Wananchi wote waliopitiwa kwenye maeneo ya mradi huu kwa mujibu wa sheria za Ardhi na fedha hizo zitatolewa mapema, pia amewaonya Wananchi watakaojitokeza kudai madai ya udanganyifu yasiyokuwa halali kwani malipo ya fidia yanahusu yule aliyekutwa na barabara na siyo aliyefuata barabara.

Awali, akiwasilisha taarifa ya mradi Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi , Mhandisi Issack Kamwelwe  amesema kwamba ujenzi  wa mradi wa Daraja la Kigongo – Busisi  utahusisha pia barabara unganishi ya lami yenye urefu wa kilomita 1.66 ambapo gharama ya ujenzi wa mradi wote utakuwa ni shilingi Bilioni 699. 2 fedha za kitanzania.

Naye Mtendaji Mkuu wa Wakala wa barabara TANROADS, Mhandisi Patrick Mfugale amesema kwamba tayari Mkandarasi toka nchini China ameshaanza kazi ya ujenzi wa daraja hili ambalo litakuwa la njia nne (4) na litajengwa kwa ubora zaidi na matarajio ya kudumu kwa zaidi miaka 100, ambapo daraja hili lina urefu wa kilomita 3.2 ambalo litakuwa daraja la kwanza kwa ukubwa kwa nchi za Afrika Mashariki na hivyo kuwa daraja la sita kwa Afrika nzima.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.