• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Naibu Waziri Kandege aipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa kutoa Mikopo ya Milioni 298 kwa Vikundi 45

Imewekwa : March 3rd, 2020

Naibu Waziri wa TAMISEMI, Josephat  Kandege  aipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi kwa  kutoa Mikopo  ya shilingi 298,117, 000 /= toka Mapato ya ndani kwa vikundi mbalimbali  vya Wanawake, Vijana na watu wenye Ulemavu kuanzia mwaka Julai 2018 hadi machi mwaka huu. .

Akizungumza na Viongozi wa ngazi ya Wilaya wakati wa ziara ya kikazi  ya kutembelea na  kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo Wilayani Misungwi, Mhe, Josephat Kandege amewapongeza Viongozi na Watendaji wote kwa juhudi na mipango thabiti katika kusimamia miradi ya Vikundi vya Vijana, Walaemavu na Wanawake inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo.

“ katika mambo ambayo nina kila sababu na nazidi kuupongeza Uongozi wa Wilaya na Halmashauri hii, ni namna ambavyo wameweza kusimamia vizuri zoezi la  utoaji wa Mikopo ya asilimia 10 ya fedha zitokanazo na mapato ya ndani, kimsingi nimesikia katika Halmashauri za Mkoa wa Mwanza, hawa ndo wamekuwa wanatoa zaidi ya  shilingi milioni 45 katika vikundi viwili, hatuwezi kuendelea kutoa shilingi milioni moja moja  ambazo haziwezi kutufikisha mbali,” alieleza kwa msisitizo Naibu Waziri Kandege.

Ametoa wito na kuwahimiza Wakurugenzi wote wa Halmashauri zingine nchini kuiga mfano wa Halmashauri ya Misungwi  katika suala la utoaji wa mikopo hii, tunatarajia mikopo hii itatoa fursa za ajira kwa vijana wengi na kuweza kuwasaidia mamilioni ya Watanzania  na kuachana na habari na utaratibu wa kutoa mikopo ya milioni moja moja ambayo haiwezi kuwasaidia Wananchi kuinua uchumi na kujikwamua na umasikini.

Mhe, Kandege amewataka  Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha mikopo ya vikundi inarejeshwa kwa wakati ili ziweze kukopeshwa kwa wengine na kuwaomba kukopesha mikopo hiyo kwa vikundi ambavyo vinaweza kufanya miradi mikubwa kama Kikundi cha Usagara Gypsum Group ambacho kinatengeneza Mikanda ya Gypsum pamoja na Chalk  Wilayani Misungwi na kuwasimamia kuwawezesha vizuri ili waweze kurejesha mikopo vizuri.

Akitoa taarifa ya Wilaya ya maendeleo ya utoaji wa Mikopo kwa vikundi Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya, Willehimina Nkunga amesema kwamba Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi, kwa kipindi cha kuanzia Julai 2018 hadi Machi 2020 imefanikiwa kutoa mikopo  kwa vikundi mbalimbali 45 vya Wanawake, Vijana na watu wenye Ulemavu wenye  shilingi milioni 298,117,000/= kwa ajili ya kuanzisha miradi ya maendeleo.

Bi, Nkunga amesema kuwa  Halmashauri imetoa mikopo katika Vikundi  45 ambavyo ni vikundi vya Wanawake 24, Vikundi vya Vijana 15, na Vikundi vya watu wenye Ulemavu 6 na kueleza kwamba wameviwezesha mikopo wa shilingi milioni 45,000,000/=  vikundi viwili vya Vijana ambavyo ni Kikundi cha Usagara Gypsum Group shilingi milioni 11,000,000/= za mradi wa Kiwanda  kidogo cha kutengeneza Mikanda ya Gypsum  pamoja na mkopo wa kununua mashine ya kutengeneza Chalk shilingi milioni 13,500,000/=, pia Kikundi cha Mabuki Vijana Maendeleo walipewa mkopo wa shilingi milioni 22,600,000/= kwa ajili ya mradi wa Kiwanda kidogo cha kusindika maziwa, ambapo uzalishaji umeshaanza tayri.

Ameongeza kuhusu marejesho ya mikopo hiyo kwa  walemavu , Wanawake na Vijana wameshaanza marejesho na kwamba  kwa vikundi vya Vijana yanaendelea vizuri na Idara ya maendeleo ya jamii inaendelea kuratibu na kufuatilia marejesho hayo na kuhakikisha yanafanyika kwa wakati.

Katika ziara ya Naibu Waziri wa TAMISEMI Mhe, Josephat Kandege  Wilayani Misungwi, ameweza kukagua na kuona shughuli za miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo na Ukarabati wa Jengo kwa ajili ya Soko la Madini, mradi wa Ufyatuaji wa matofali wa Halmashauri, mradi wa Kiwanda cha kutengeneza mikanda ya Gypsum na Chalk Usagara, mradi wa barabara ya Nyashishi – Fella ambapo ameridhishwa na kazi zinazoendelea.


Mmoja wa Wanakikundi wa Kikundi cha Usagara Gypsum Group kinachotengeneza Mikanda ya Gypsum akiandaa Nyuzi kwa ajili ya kutengeneza mkanda wa Gypsum wakati Mhe, Naibu Wazuri wa TAMISEMI alipotembelea kuona shughuli za kikundi hicho eneo la Usagara Wilayani Misungwi.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.