• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

DC Misungwi aagiza Watendaji kukusanya Ushuru wa Madini ya Dhahabu na Almasi

Imewekwa : September 25th, 2018

MKUU WA WILAYA  AAGIZA  WATENDAJI WA HALMASHAURI KUKUSANYA  MAPATO YA USHURU WA MADINI YA DHAHABU NA ALMASI

Mkuu wa Wilaya ya Misungwi, Mhe,Juma Sweda amewataka Watendaji wa Halmashauri kufuatilia na  kuhakikisha wanakusanya Mapato yanayotokana na Ushuru wa Huduma kutoka kwa Makampuni yanayofanya shughuli za Uchimbaji na Uchenjuaji wa Madini ya Dhahabu na Almasi katika Migodi iliyopo maeneo ya Ishokela na Mwanagwa Wilayani humu.

Akizungumza na Menejimenti ya Halmashauri mapema leo Mhe, Mkuu wa Wilaya ya Misungwi amewaagiza Wakuu wa Idara na Vitengo kuhakikisha kwamba Mapato hayo yanayotokana na Ushuru wa Huduma yanakusanywa kutoka  kwa Makampuni yote yanayojishughulisha na Uchimbaji na uchenjuaji wa Madini ya dhahabu na Almasi katika  maeneo mbalimbali kwa kipindi chote ambacho hawajalipa ili kuweza kuboresha na kuongeza Makusanyo ya Mapato ya ndani ya Halmashauri.

Mhe,Juma Sweda amesema kuwa Wamiliki wa Makampuni ya Uchimbaji na Uchenjuaji  yote yanayofanya kazi katika maeneo ya Ishokela, Mwamazengo, Shilalo, Mwanangwa na Mabuki yanapaswa kulipa Mapato ya Ushuru wa Huduma kwa Halmashauri wanapofanyia kazi na kwa mujibu wa takwimu zilizopo Makampuni hayo hayalipi kabisa na matokeo yake Halmashauri imepoteza Mapato hayo kwa muda mrefu sasa, na kuwataka Watendaji wafuatilie na kuhakikisha wote wanalipa Ushuru wa mwaka 2018/2019 pamoja na madeni yote ya nyuma.

Ameeleza kuwa ameweka Mikakati ya kuyafungia kufanya kazi ya Uchimbaji Makampuni ambayo yatashindwa kukamilisha malipo ya Ushuru husika na kuwaomba Wamiliki hao kulipa mapema vinginevyo hatua za Kisheria zitachukuliwa dhidi yao pamoja na kufungiwa kufanya shughuli za uchimbaji katika maeneo yote ya Wilaya ya Misungwi.

Mhe,Juma Sweda amewataka pia Watendaji wa Halmashauri ya Misungwi kufanya kazi kwa uaminifu, uadilifu wa hali ya juu pamoja kutekeleza majukumu yao kwa Weledi kwa lengo la kuleta ufanisi na kuongeza tija kazini hususan katika suala la kuongeza na kuimarisha ukusanyaji wa Mapato ya vyanzo vya ndani kwa njia ya Kielektroniki pamoja na kusimamia utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya maendeleo inayofadhiliwa na Serikali na Wadau wengine kupitia Sekta ya Afya,  Elimu, Maji, Kilimo, Mifugo na Uvuvi, TASAF III, miundombinu na Maendeleo ya Jamii kwenye miradi ya Vikundi vya Wanawake ,Vijana na Wenye Ulemavu.

Ameagiza Wakuu wa Idara na Vitengo kwenda Vijijini kutembelea na kusimamia  miradi ya maendeleo ya Sekta mbalimbali inayoendelea kutekelezwa na mingine ipo katika hatua za ukamilishaji na kuweza kushauri na kushirikiana na Wananchi katika shughuli za ujenzi wa miradi husika na kuhakikisha inakamilika kwa wakati kwa kuzingatia ubora na viwango vya kitaalamu kwa  kufuata sheria, taratibu na kanuni na miradi itekelezwe na kukamilika  kulingana  na thamani ya fedha husika.

Mhe, Sweda amewataka Watendaji wote kutekeleza kikamilifu maelekezo na maagizo yanayotolewa na Viongozi wa Serikali na kuwakumbusha kuhusu maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe, Dkt, John Pombe Joseph Magufuli na Makamu wa Rais Mhe, Samia Suluhu Hassan ya Wanancchi wote kufanya Usafi wa mazingira katika maeneo ya biashara na maofisini pamoja na kufanya Mazoezi ya Viungo kwa ajili ya kulinda afya na kujikinga na Magonjwa mbalimbali yasiyo ya kuambukiza , ambapo kila Mtumishi na Mwananchi anatakiwa kutekeleza maelekezo hayo kila Jumamosi ya pili pamoja na kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi,” nahitaji maelekezo hayo yaendelee kutekelezwa kwa kila Mkuu wa Idara na Vitengo kuwakumbusha Watumishi wake na Afisa Utumishi ahakikishe utekelezaji unafanyika katika Kata zote 27 kuanzia mwisho wa mwezi huu Septemba 2018 Watumishi wote wabadilike na kutimiza wajibu wao”.  Alisisitiza Mkuu wa Wilaya, Juma Sweda.

Awali, katika mazungumzo yake amezitaka Idara na Vitengo vya  Halmashauri kuwa na mpango madhubuti wa kutoa taarifa kwa Wananchi kupitia vyombo mbalimbali vya Habari kuhusu mafanikio ya utekelezaji wa shughuli na miradi mbalimbali ya maendeleo inayoendelea kujengwa na iliyokamilika ili Wananchi waweze kuona namna Serikali ya awamu ya tano  inavyotekeleza na kuwapatia maendeleo ya  kiuchumi na kijamii.

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DC Misungwi awataka Wananchi wa Kijiji cha Ibinza kata ya Isenengeja kudumisha amani na mshikamano.

    May 22, 2025
  • DC Misungwi akabidhi Vifaa saidizi vya Vitimwendo 15, Jezi na Mipira kwa Wanafunzi na Watoto wenye ulemavu kukwa Shule za msingi 16.

    May 21, 2025
  • Misungwi yapongeza kwa upatikanaji wa Mitambo ya kuondoa magugu maji itakayowasili mwishoni mwa mwezi julai 2025

    May 19, 2025
  • DC Misungwi awapongeza Waalimu wa Shule za Sekondari kwa ufaulu wa Asilimia 99.75

    May 16, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.