• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Ardhi na Maliasili
      • Utawala na Raslimali Watu
      • Mipango na Takwimu
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Idara ya Ujenzi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Maji
      • Fedha na Biashara
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Uchaguzi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Ufugaji Nyuki
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Maeneo ya Vivutio vya Utalii
    • Maeneo ya Kilimo
    • Maeneo ya Madini
    • Maeneo ya Uwekezaji wa Mazingira
  • Huduma Zetu
    • Huduma Sekta ya Afya
    • Huduma Sekta ya Elimu
    • Huduma Sekta ya Maji
    • Huduma Sekta ya Mazingira
    • Huduma Sekta ya Maendeleo ya Jamii
    • Huduma Sekta ya Ardhi na Maliasili
  • Baraza la Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Kamati ya Huduma za Uchumi na Mazingira
      • Kamati ya Kudhibiti Ukimwi
      • Kamati ya Huduma za Kijamii
      • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba Vikao vya Halmashauri
  • Miradi mbalimbali
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Mbalimbali
    • Taratibu
    • Gazeti la Serikali
    • Taarifa
    • Fomu mbalimbali
    • Zabuni
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Video Mpya
    • Maktaba ya Picha
    • Habari Mpya

Baraza la Madiwani lafukuza Watumishi 7 kwa utoro, wengine wanne warejeshwa kazini Misungwi

Imewekwa : September 16th, 2021

Watumishi saba (7) wafukuzwa kazi kutokana na tuhuma za utoro na kukiuka kanuni za utumishi wa umma  katika Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi , Mkoani Mwanza.

Mamauzi hayo yalitolewa na Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi  katika Mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Halmashauri hiyo jana, ambapo Mwenyekiti wa Halamshauri hiyo Mhe, Kashinje Machibya alieleza kwamba Halmashauari  imeridhia uamuzi wa Tume ya uchunguzi ambayo ilipitia mashitaka na kutoa uamuzi wa Watumishi 7 kufukuzwa kazi na wengine wannne kurejesha kazini.

Mhe, Machibya amesema kwamba sababu za  kufukuzwa  kazi Watumishi hao ni kutokana na kuwa na tuhuma mbalimbali za kiutumishi ikwemo utoro kazini zaidi ya siku tano, udagannyifu na kugushi vyeti vya kidato cha Nne, pamoja na upotevu wa fedha za ushuru wa mapato ya Halmashauri.

Mhe, Machibya ameeleza na kutoa Wito kwa Watumishi wengine kufanya kazi kwa weledi na kuzingatia kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma na  kuwataka kuzingatia kanuni na maadili ya kazi na kwamba wao kama Baraza hawafurahishwi na kitendo cha Mtumishi kuondolewa kazini hivyo waendelee kuwajibika kikamilifu.

Aliongeza kwamba Halmashauri kwa kipindi cha kuishia Julai 2021 imekuwa na usimamizi mzuri katika matumizi ya fedha za Umma ambapo imefanikiwa kuwa na Hati safi katika ukaguzi wa Hesabu za mwaka 2019/2020 zilizofanywa na Mdhibiti na Mkaguzi  Mkuu wa Serikali na kuwapongeza Madiwani wote, viongozi wa Serikali pamoja na Menejimenti kwa ujumla kwa ushirikiano wakati wote.

Kwa mujibu wa taarifa ya Tume ya uchunguzi ilibainisha Watumishi 7 waliofukuzwa kazi ni pamoja na; Alphonce Samula Madukulu ambaye ni Mlinzi kwa kosa la utoro  Ernest Msiba Celestine,Daktari wa Kituo cha Afya Misasi kwa kosa la utoro kazini, Wilson S. Alilah aliyekuwa Daktari, kwa mashitaka ya kosa la utoro kazini  Hilary W. Mtui ambaye alikuwa Daktari katika Hospitali ya Wilaya ya Misungwi kwa kosa la utoro,  Simon Makanga Wilson  aliyekuwa Afisa Muuguzi msaidizi  katika Zahanati ya Nkinga kwa kosa la utoro kazini , Rozalio Kipondya Aloyce, ambaye ni Mtendaji wa Kijiji cha Seeke kwa kosa la upotevu wa mapato ya ndani shilingi Milioni 3,897,500/=, Bernard Joseph Makungwi, aliyekuwa Dereva wa Halmashauri kwa kosa la kudaganya elimu ya kidato cha Nne.

Pia taarifa hiyo ilieleza kuhusu Watumishi wanne Waliorejeshwa kazini ambao ni pamoja na John Shuka Mathias,ambaye ni Mtendaji wa Kijiji cha Mahando kwa kosa la utoro kazini, Maganya Shemu Kiyoya, Mtendaji wa Kijiji cha Lubili kwa kosa la utoro , na Godfrey H. Malogo ambaye ni Mtendaji wa Kata ambaye atapelekwa Mahakamani kwa kosa la upotevu wa mapato ya ndani ya shilingi Milioni 1,520,150/=, na George A. Sanga ambaye ni Dereva kwa kosa la kutotii mamlaka ambaye iliamuliwa apunguzwe mshahara kwa asilimia 15 kwa kila mwezi  kwa miaka mitatu mfululizo.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Misungwi Bi. Leokadia Humera amekiri kuwepo kwa maamuzi hayo ya Baraza la Madiwani ya kuwafukuza kazi Watumishi hao saba na kuwarejesha kazini Watumishi 4 kati ya 11 waliokuwa na mashitaka mbalimbali ya kiutumishi ambapo Tume iliundwa kuchunguza tuhuma zao kulingana na makosa waliyotenda na kuwasilisha taarifa katika mkutano wa Baraza la Madiwani uliopita.

Bi. Leokadia Humera amesema kwamba Halmashauri katika kipndi cha kuishia mwezi Julai 2021 imefanikiwa kukusanya fedha za mapato ya ndani yenye jumla ya shilingi Bilioni 2, 365, 911, 590.40 sawa na asilimia 102.87,  na kutekeleza miradi ya maendeleo yenye jumla shilingi Bilioni 39, 310, 714,034.03 sawa na asilimia 89.12.ambapo miradi hiyo imekamilika na mingine inaendelea kukamilishwa.

Alifafanua mafanikio yaliyopatikana katika kipindi hicho ni pamoja na; ujenzi wa Kituo cha Afya cha Koromije ambacho kwa sasa kinatoa huduma za upasuaji pamoja na ujenzi majengo mawili katika Hospitali ya wilaya ya Misungwi. sambamba na ujenzi wa madarasa 26 vya madarasa, nyumba 3 za walimu pamoja na matundu 78 ya vyoo katika shule za msingi na kwa upande wa sekondari Halmashauri imefanikiwa kujenga vyumba 10 vya madarasa, maabara za Sayansi 3, na bweni 1 la wanafunzi wa kike katika Sekondari ya Misungwi.

 Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Misungwi Mhe. Kashinje Machibya (wa pili kulia), akifatiwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi Bi.Leokadia Humera pamoja na viongozi wengine wa chama cha Mapinduzi (CCM) wakisikiliza na kufatilia mjadala katika mkutano wa Baraza la Madiwani Wilaya ya Misungwi.

 Baadhi ya Madiwani wakiufatilia mjadala kwa umakini katika mkutano wa Barazala Madiwani  katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi.


                                                                                                                          

Matangazo

  • SHULE ZILIZOVUNJA REKODI KATIKA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MWAKA 2024 February 01, 2025
  • TANGAZO ZABUNI UPANGISHAJI VIBANDA VYA HALMASHAURI MWAKA 2023/2024 June 28, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 20, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE WA JIMBO LA MBARALI NA MADIWANI KATIKA KATA SITA ZA TANZANIA August 10, 2023
  • Angalia yote

Habari Mpya

  • DAS Misungwi awapongeza Watendaji Halmashauri kwa kushirikiana na Madiwani katika kuongeza ufanisi na ukusanyaji wa Mapato.

    April 29, 2025
  • Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi yafanya ziara ya yatembelea na kupata mafunzo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya nyang'hwale Mkoani Geita

    April 25, 2025
  • Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango yaridhishwa na miradi ya maendeleo ya Halmashauri Wilaya ya Misungwi

    April 23, 2025
  • Kamati ya Lishe ya Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi yawataka Watendaji wa Kata na Vijiji kutoa Elimu ya Shughuli za Lishe kwa Wananchi.

    February 27, 2025
  • Angalia yote

Video

Uzinduzi wa Tovuti za Mikoa pamoja na Halmashauri
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Takwimu za wanafunzi kitaifa
  • Taarifa
  • Kujisajili chama cha Mapinduzi-ccm
  • MFUMO WA UJAZAJI MATAMKO KWA NJIA YA MTANDAO
  • KUPATA KIUNGANISHI CHA MFUMO WA TAARIFA ZA SHULE-SIS
  • Historia ya Halmashauri
  • Sheria Mbalimbali
  • Wasiliana Nasi
  • Malalamiko

Viunganishi Linganishi

  • Ikulu
  • Utumishi
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Tamisemi
  • Mwanza Region
  • Wakala wa Serikali Mtandao (Ega)

Ramani ya Wasomaji

world map hits counter

Wasomaji

freevisitorcounters's Website

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Halmashauri ya Wilaya Misungwi

    Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI

    Simu ya Mezani: +255282983268

    Simu ya Mkononi: 0717259106

    Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.