Katibu Tawala Wilaya ya Misungwi Bw. Abdi Makange amewataka Viongozi na Watendaji wa Serikali kuongeza ushirikiano na bidii katika Ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashuri ili kukuza uchumi na kuimarisha shunguli za jamii wilayani Misungwi Mkoani Mwanza.
Akizungumza wakati wa kikao maalum cha Kamati ya ushauri Wilaya tarehe 21 Januari 2025 Bw. Makange kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Misungwi Mhe. Johari Samizi amehimiza Viongozi na Watendaji wote kuendelea kusimamia na kukusanya mapato ya ndani ya Halmashauri ili kuweza kutimiza malengo yaliyowekwa kwenya Bajjeti za kila mwaka na amewapongeza wajumbe kwa ushiriki wao na kusisitiza kuwa mawazo yote yaliotolewa yatafanyiwa kazi ambapo ushirikiano thabiti unatakiwa kufanyika ili bajeti hiyo itekelezwe ikiwa ni pamoja na kuimarisha na kutekeleza kikamilifu miradi ya maendeleo.
Awali akiwasilisha rasimu ya Bajeti ya mwaka 2025/2026 iliyokadiriwa shilingi Bilioni 53,614,834,111/= Afisa Mipango wa Halmashauri Bi. Peniel Titus amefafanua kwamba katika rasimu hiyo ya Bajeti kiasi cha shilingi 4,641,245,829/= ni fedha zitokanazo na vyanzo vya Mapato ya ndani ya Halmashauri ,kiasi cha shilingi. Bilioni 41,888,608,000/= ni fedha ya mishahara ya Watumishi, na kiasi cha shilingi Bilioni 1,359,841,000/= ikiwa ni ruzuku ya uendeshaji ( OC) na kiasi cha shilingi Bilioni 5,725,139,282/= ni kwa ajili ya kutekeleza Miradi ya Maendeleo na fedha zote ni kutoka Serikali kuu.
Bi. Peniel Titus ameeleza kuwa pamoja na kuwepo kwa rasimu ya bajeti hiyo ofisi ya Mipango na Uratibu imeahidi kutekeleza na kufanyia kazi mapendekezo na maadhimio ya kikao hicho kama ambavyo wajumbe wameshauri ikiwa ni pamoja na kuyapokea na kuyatekeleza ili kuhakikisha kuwa na maendeleo chanya katika jamii ndani ya Halmashauri ya Misungwi na kueleza kuwa makadirio ya Bajjeti hiyo yamelenga Zaidi kuongeza ustawi kwa jamii kupitia utekelezaji wa miradi ya maendelo na ukusanyaji wa Mapato ya ndani.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Misungwi Bw. Addo Missama kuwa kikao hicho ni maalum kwa ajili ya kupitia na kufanya tathmini ya utendaji kazi ambapo kwa bajeti hiyo 2025/2026 atahakikisha inatekelezwa na kufanyiwa kazi akishirikiana na Wakuu wa Taasisi za umma, Wakuu wa Idara na Vitengo vya Halmashauri ya Misungwi ili kutimiza malengo yaliyopangwa ili kufanikisha maadhimio na hatimaye kujiandaa na utekelezaji wa shughuli za kimaendeleo katika Halmashauri.
Naye Meneja wa Wakala wa Barabara za mjini na Vijijini (TARURA) Wilaya ya Misungwi Mhandisi Kassim Shabani wakati akiwasilisha taarifa ya bajeti ya matengenezwwo ya Barabara amesema kuwa Misungwi ima mtandao wa barabara zilizosajiliwa na zenye urefu wa kilometa 927.54 km zilizogawanyika katika makundi na viwango vya lami,changarawe na udongo ambapo kwa mwaka wa fedha 2025/20226 TARURA inategemea kutengewa kiasi cha shilingi Bilioni 2,235,430,000/= kutoka Serikali kuu ambayo ni Tozo za mafuta, mfuko wa barabara na Mfuko wa Jimbo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wajumbe wa kikao hicho akiwemo Bi. Agness Kapingu ambaye ni Mtafiti kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo TARI Ukiriguru amepongeza juhudi zinazofanywa na Halmashauri hiyo ambapo ametoa mapendekezo na kushauri kuhusu suala la utojia elimu endelevu kwa wakulima na wafugaji ili kukuza uelewa na kuwapa fursa zaidi katika sekta ya kilimo na uvuvi pamoja na Bw. Mussa Mwika ambaye ni Mwakilishi wa vyama vya siasa alishauri na kupendekeza kwamba Halmashauri iendelee kuweka mipango mizuri ya maendeleo ikiwemo kukamilisha ujenzi wa choo katika soko kuu la Misungwi na kutenga eneo la maegesho ya magari ili kuongeza mapato ya ndani.
Katika kikao hicho maalum cha Bajeti kilichowashirikisha wajumbe ambao ni pamoja na Viongozi wa Vyama vya siasa,Viongozi wa Dini, Wakuu wa Taasisi za umma, Wakuu wa Idara na Vitengo vya Halmashauri ya Misungwi kwa ujumla wao walijadili na kutoa mapendekezo ya kina.
Halmashauri ya Wilaya Misungwi
Sanduku la Posta: P.O Box 20 MISUNGWI
Simu ya Mezani: +255282983268
Simu ya Mkononi: 0717259106
Barua Pepe: ded@misungwidc.go.tz
Copyright ©2021 Misungwi District Council . All rights reserved.